1. Kabla ya kuanza safari (yaani kusafiri kwenda sehemu ambayo ni kilomita 78 au zaidi), mtu anatakiwa kuswali rakaa mbili. Swalaah hii inajulikana kama Swalaatus Safar.
Mut’im bin Miqdaam (rahimahullah) anasimulia kwamba Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Hakuna kitendo ambacho mtu anaweza kukiacha pamoja na familia yake kabla ya kuanza safari ambayo ni kheri zaidi kuliko rakaa mbili (Swalatus Safar) watakayoiswali.”
Imepokewa kwamba wakati wowote Ibnu Umar (Radhiyallahu anhuma) alipokusudia kuanza safari, alikuwa anaenda msikitini kwanza na kuswali.
2. Kutana na wanafamilia na marafiki zako kabla ya kuanza safari (kama unaposafiri kwa ajili ya umrah au hajj) na uwaombe wakuombee dua.
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraira (Radhiyallahu anhu) kwamba Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Mmoja wenu anapotaka kusafiri basi anapaswa kukutana na ndugu zake Waislamu (yaani familia na marafiki na kuomba wamuombee dua). Hakika dua yao iliyoongezwa pamoja na dua yake itakuwa ni njia ya yeye kupata wema (wakati wa safari yake).
3. Wajulishe familia yako sehemu unapokwenda na mahali unapoishi wakati wa safari yako ili iwe rahisi kwao kuwasiliana nawewe.
Alislaam Juhudi za Kuleta uislam ndani ya maisha yetu