Sunna na Adabu

Sunna na Aadaab za Jumu’ah 2

6. Ni vizuri kuvaa nguo nyeupe. Imepokewa kutoka kwa Ibnu Abbaas (radhiyallahu anhuma) kwamba Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Vaa nguo nyeupe, kwa sababu hiyo ni nguo bora kabisa, na wafunike humo marehemu zenu.” 7. Imepokewa kwamba Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) wakati fulani alikuwa akisoma Surah Sajdah katika rakaa ya …

Soma Zaidi »

Sunna na Aadaab za Jumu’ah 1

1. Soma Surah Dukhan siku ya Alhamisi usiku. Imepokewa kutoka kwa Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) kuwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Mwenye kusoma Surah Haa-mim Ad Dukhaan usiku wa kuamkia Alhamis atasamehewa madhambi yake.”[1] 2. Oga (fanya ghusl) siku ya Ijumaa. Yule ambaye ataoga siku ya Ijumaa, madhambi yake madogo …

Soma Zaidi »

Fadhila za Jumu’ah 2

Siku Ambayo Ina Muda Maalum wa Kukubalika Anas bin Maalik (radhiyallahu anhu) anaripoti: Siku ya Jumu’ah iliwasilishwa kwa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam). Jibreel (alaihis salaam) alikuja kwa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam). Katika kiganja chake kulikuwa na kitu kinachofanana na kioo cheupe, na katikati ya kioo kulikuwa na doa jeusi. Mtume …

Soma Zaidi »

Fadhila za Jumu’ah

Kusamehewa Madhambi Kwa Kuswali Jumu’ah Imepokewa kutoka kwa Abu Hurairah (radhiyallahu anhu) kwamba Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Madhambi yaliyotendwa baina ya Jumu’ah mbili, maadamu si madhambi makubwa, yatasamehewa na Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’alah) (kwa kuswali Jumu’ah zote mbili).[1] Siku Maalum ya Waumini Ibnu Abbaas (radhiyallahu anhuma) anasimulia kwamba Mtume …

Soma Zaidi »

Jumu’ah

Siku ya Jumu’ah ina umuhimu mkubwa katika Uislamu. Ni miongoni mwa neema kubwa za Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’alah) juu ya ummah huu ni sifa adhimu ya Uislamu. Amesema Mtume (sallallahu alaihi wasallam): “Siku ya Jumu’ah ni sayyidul ayyaam (yaani kiongozi wa siku zote na ni siku kubwa zaidi (kuliko siku …

Soma Zaidi »

Sunnat Na Adabu Za Kuamkiana (Kutoa Salaam) 8

28. Waislamu wawili wanapokutana, basi baada ya kutoa salamu, wafanye musaafahah (wapeane mikono). Imepokewa kutoka kwa Abdullah bin Mas’uud (radhiyallahu anhu) kwamba Mtume (sallallahu alaihi wasallam) amesema: “(Wanapokutana Waislamu wawili basi) ukamilisho wa maamkiano yao ni kwamba wafanye musaafahah wao kwa wao.”[1] 29. Wakati wa kufanya musaafaha ni sunna kufanya …

Soma Zaidi »

Sunnat Na Adabu Za Kuamkiana (Kutoa Salaam) 7

26. Ni adabu kwamba mtu anapotembea na mwingine amekaa, basi anayetembea aanze kutoa salamu wa kwanza. Vile vile, wakati mtu mmoja anapopanda mnyama na mtu mwingine anatembea, basi yule ambaye kampanda mnyama aanze kutoa salamu wa kwanza. Na hivyo, vijana wanapaswa kuwasalimia wazee kwanza, na kikundi kidogo (wale ambao ni …

Soma Zaidi »

Sunnat Na Adabu Za Kuamkiana (Kutoa Salaam) 6

18. Ukiingia kwenye mkusanyiko wenye mazungumzo au majadiliano ya Dini inafanyika, hupaswi kutoa salaam kwa sababu hili litamsumbua mwenye kuongea pamoja na wale waliohudhuria mkusanyiko huo. 19. Ikiwa mtu amezama katika mazungumzo au anajihusisha na baadhi ya mambo basi ni bora mtu asimsalimie. Lakini, ikiwa mtu anajua kwamba hatokuwa na …

Soma Zaidi »

Sunnat Na Adabu Za Kuamkiana (Kutoa Salaam) 5

13. Unapotoka nyumbani, toka nyumbani na salamu. Qataadah (radhiyallahu anhu) ameripoti kuwa Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Mkiingia nyumbani, basi wapeni salamu waliomo ndani yake, na unapotoka (nyumbani), basi acha salamu yako kama amana kwa watu wa nyumbani kwako (yaani salamu kwa watu unapoondoka).”[1] Maelezo: Nabii (sallallahu alaihi wasallam) ametufundisha …

Soma Zaidi »