Monthly Archives: February 2024

Sunna Na Adabu Za Dua 7

17. Ni bora kuomba dua pana. Aaishah (radhiyallahu ‘anha) anaripoti kwamba Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) alikuwa akipendelea dua hizo ambazo ni pana na alikuwa akiacha dua zingine. Dua hizi zifuatayo ni miongoni mwa dua za Masnoon ambazo zimepokelewa katika Hadith: رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ …

Soma Zaidi »

Damu Ya Kwanza iliyomwagika kwa ajili ya Uislamu

Muhammad bin Ishaaq (rahimahullah) anasimulia: Mwanzoni katika Uislamu, Maswahaabah wa Mtume (Sallallahu ‘alaihi wasallam) walikuwa wakiswali kwa siri. Walikuwa wakienda kwenye mabonde ya Makka Mukarramah kuswali ili Swalah zao zibaki siri kwa makafiri (na ili waokoke na mateso ya makafiri). Wakati mmoja, wakati Sa’d (Radhiya Allaahu ‘anhu) alikuwepo pamoja na …

Soma Zaidi »

Sunna Na Adabu Za Dua 6

15. Usiombe dua kwa jambo lolote lisiloruhusiwa au kwa chochote kisichowezekana (kama mtu kuomba kuwa Nabi). Imepokewa kutoka kwa Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) kwamba Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) amesema: “Dua ya mtu itakubaliwa daima maadamu haombi kitu cha dhambi au kukata mahusiano ya kifamilia, na maadamu hana haraka (katika dua …

Soma Zaidi »

Uislamu Unakaribisha Nini?

Katika zama za Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam), watu mbalimbali walianza kusilimu. Ujumbe wa Uislamu ulipoenea na kufikia maeneo mbalimbali, Aksam bin Saifi (rahimahullah), kiongozi wa ukoo wa Tameem, alipendezwa na kujua kuhusu Uislamu. Kwa hiyo, aliwatuma watu wawili kutoka katika kabila lake kusafiri kwenda Madinah Munawwarah ili kufanya utafiti kuhusu …

Soma Zaidi »

Upendo Kwa Answaar

‘Aamir (rahimahullah), mtoto wa Sa’d (radhiya allaahu ‘anhu), anasimulia yafuatayo: Wakati fulani nilimwambia baba yangu, “Ewe baba yangu mpendwa! Ninaona kwamba unaonyesha upendo na heshima ya ziada kwa Answaar ikilinganishwa na watu wengine.” Sa’d (radhiya allaahu ‘anhu) akaniuliza, “Ewe mwanangu! Hujafurahishwa na hili?” Nikamjibu, “Hapana! Sina furaha. Lakini, nimefurahishwa sana …

Soma Zaidi »

Sunna Na Adabu Za Dua 5

12. Baada ya kumaliza dua yako, sema aameen. Abu Musabbih Al-Maqraaiy anasimulia: Wakati mmoja, tulikuwa tumekaa na Abu Zuhair An-Numairi ambaye alikuwa miongoni mwa maswahaabah (radhiyallahu anhum). Alikuwa mfasaha zaidi katika lugha. Wakati mtu yoyote miongoni mwetu alikuwa akishiriki katika dua, alikuwa akisema: “ufunge dua hiyo kwa Aamin, kwa sababu …

Soma Zaidi »

Utabiri Wa Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) kuhusiana na Sa’d (radhiya allaahu ‘anhu) Kushinda Qaadisiyyah

Katika tukio la Hajjatul Wadaa’, Sa’d (Radhiyallahu ‘anhu) alikuwa ameumwa huko Makka Mukarramah na alihofia kwamba angeaga dunia. Rasulullah (Sallallahu ‘alaihi wasallam) alipokuja kumtembelea, alianza kulia. Rasulullah (Sallallahu ‘alaihi wasallam) akamuuliza: “Kwa nini unalia?” Sa’d (Radhiya Allaahu ‘anhu) akajibu, “Nahofia kuwa nitafariki katika ardhi ambayo niliifanya Hijrah, na kwa kufariki …

Soma Zaidi »

Sunna Na Adabu Za Dua 4

9. Wakati wa kuomba dua, moyo wako unapaswa kulenga kikamilifu na makini kwa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’aala). Moyo wako usiwe umeghafilika na kutojali wakati wa omba dua. Hupaswi kuangalia huku na huku na kuwangalia watu pindi unapoomba dua. Imepokewa kutoka kwa Abu Huraira (radhiyallahu ‘anhu) kwamba Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) …

Soma Zaidi »

Khutba Ya Kwanza Huko Madina Munawwarah baada ya Hijrah

Katika tukio la hijra, wakati Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) alipoingia kwenye mji uliobarikiwa wa Madinah Munawwarah, watu wengi walikuwa wakimgojea kwa hamu. Miongoni mwao walikuwemo wale wanaompenda Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) -Ansaar wa Madinah Munawwarah – pamoja na Mayahudi na wale wanao abudu masanamu waliokuwa wakiishi katika mji huo. Rasulullah …

Soma Zaidi »

Uthabiti wa Sa’d (Radhiyallahu ‘anhu) Kwenye Imaan Yake

Abu ‘Uthmaan (Rahimahullah) anasimulia kwamba Sa’d (Radhiya Allaahu ‘anhu) alisema: Aya ifuatayo ya Qur’an tukufu iliteremshwa kunihusu mimi: وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حُسْنًا ۖ وَإِن جَاهَدَاكَ لِتُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا Tumemuusia mwanaadamu kuwafanyia wema wazazi wawili. Na wakikulazimisha (wazazi wako makafiri) kunishirikisha (katika ibada yangu) yale …

Soma Zaidi »