
Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Mwenye kufa kwa tauni kafa kama shaheed.
Wakati wa ukhalifa wa Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu), tauni la Amwaas uliathiri Shaam ndani ya mwaka wa 17 baada ya Hijrah. Katika tauni hii, Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu), kiongozi wa Waislamu huko Shaam, alipatwa na tauni hiyo na baadae akafa. Kabla ya kufariki, alimteua Mu’aaz bin Jabal (Radhiya Allaahu ‘anhu) kuwa mrithi wake.
Mu’aaz bin Jabal (Radhiya Allaahu ‘anhu) akawahutubia watu na kutoa khutba ifuatayo, “Enyi Watu! Tauni ni rahma kwenu. Ilikuwa ni dua ya Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) na ilikuwa ni sababu ya wachamungu kufariki! Hakika Mu’aaz anamwomba Allah Ta’ala amjaalie yeye na familia yake sehemu katika tauni.”
Muda mfupi baadaye, niliporudi nyumbani kutoka Msikitini, Mu’aaz (Radhiya Allaahu ‘anhu) aligundua kuwa mwanaye ni mgonjwa na alipatwa na tauni. Aliendelea kumtunza na kumuuguza hadi alipofariki dunia.
Kulingana na baadhi ya masimulizi, mabinti zake wawili pia walifariki kwa tauni hiyo.
Baada ya hapo, Mu’aaz (Radhiya Allaahu ‘anhu) mwenyewe aliugua wakati wa tauni na akafariki. Mwanzoni mwa ugonjwa wake, alipoona vidonda vinaonekana kwenye mkono wake, ambavyo vilikuwa ni dalili za tauni, alisema kwa furaha huku akiuangalia mkono wake, “Siko tayari kubadilishana (sehemu ya tauni iliyonipata) kwa hata ngamia wekundu (wa kiarabu ambao walizingatiwa kama utajiri wa thamani sana kwa mujibu wa Waarabu)!”
Baada ya hapo, Mu’aaz (Radhiya Allaahu ‘anhu) naye akaaga dunia.
(Kashful Astaar #3042, Al Bidaayah wan Nihaayah 10/43, At Tabaqaatul Kubra 3/441, Siyaru A’laamin Nubalaa 3/288)
Alislaam Juhudi za Kuleta uislam ndani ya maisha yetu