Zoezi la Mu’az (Radhiyallahu ‘anhu) la Kusoma Qur’ani Tukufu ndani ya Tahajjud

Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alimtuma Mu’aaz (Radhiya Allaahu ‘anhu) kutawala sehemu fulani ya Yemen, na akamtuma Abu Musa Ash’ari (Radhiya Allaahu ‘anhu) kutawala sehemu nyingine ya Yemen.

Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) aliwahutubia na akawapa nasaha zifuatazo kabla ya kuwatuma. Akawaambia, “Rahisisheni mambo (kwa ajili ya watu), wala msifanye mambo kuwa magumu (kwa watu). Wape bishara (watu), wala usifanye mambo ambayo yatawatoa watu (katika Dini).

Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) kwanza alimtuma Abu Musa Ash’ari (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwenda Yemen, na baada ya hapo akamtuma Mu’aaz (Radhiyallahu ‘anhu) kwenda Yemen.

Walipokuwa wakiishi Yemen, Sahaabah hawa wawili walikuja kutembeleana, hasa wakati wa kusafiri kupita maeneo ya mmoja wao.

Wakati mmoja, wakati Mu’aaz bin Jabal (Radhiya Allaahu anhu) alipokuwa akipita kwenye eneo la Abu Musa Ash’ari (Radhiya Allaahu ‘anhu), alisimama kukutana naye. Baada ya kukutana, wote wawili walikaa na kujadili utaratibu wao wa kila siku wa kusoma Quraan Majeed.

Mu’aaz bin Jabal (Radhiya Allaahu ‘anhu) alimuuliza Abu Musa Ash’ari (Radhiya Allaahu ‘anhu), “Ewe Abdullah (Abu Musa), una utaratibu gani wa kusoma Quraan kila siku?

Akajibu: “Wakati wowote ninaopata kusoma Qur’an (usiku na mchana), mimi huisoma (yaani kila wakati ninapoweza kusoma Qur’an Majeed, nasoma).”

Abu Musa (Radhiya Allaahu ‘anhu) kisha akamuuliza Mu’aaz (Radhiya Allaahu ‘anhu), “una utaratibu gani wa kusoma Quraan kila siku?”

Mu’aaz (Radhiya Allaahu ‘anhu) akajibu, “Mimi nalala sehemu ya kwanza ya usiku, kisha namka (kusoma Quraan Majeed) baada ya kutimiza kiasi cha usingizi ninachohitaji. Kisha nasoma kiasi chochote (cha Quraan) Atakachoniandikia Mwenyezi Mungu nisome (wakati huo). Kama vile ninavyotarajia kupata malipo kutoka kwa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) kwa kusimama katika Swalah (wakati wa usiku na kusoma Qur-aan Majeed), hali kadhalika nina matumaini ya kupata malipo kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa usingizi wangu (wakati wa usiku, kwa sababu usingizi wangu ni kwa ajili ya kupata nguvu za kutekeleza ibaada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu subhaanahu wata’ala mchana na usiku).

About admin

Check Also

Sifa Nzuri za Muaz bin Jabal (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Farwah bin Nawfal anasimulia kwamba wakati mmoja, Abdullah bin Masoud (Radhiyallahu anhu) aliwahi kuzungumza kuhusu …