
Farwah bin Nawfal anasimulia kwamba wakati mmoja, Abdullah bin Masoud (Radhiyallahu anhu) aliwahi kuzungumza kuhusu Muaaz bin Jabal (Radhiyallahu ‘anhu) na akamsifu sana kwa wema aliokuwa nao Akisema:
إن معاذا كان أمة قانتا لله حنيفا
“Muaaz alikuwa ni ummah (kiongozi anayewaongoza wengine kwenye njia iliyonyooka), wakati yeye mwenyewe alikuwa amejitolea kikamilifu katika ibada na utiifu kwa Allah Ta’ala, na alibaki imara juu ya njia iliyonyooka, bila ya kupinda kwa njia yoyote ile.”
Farwah bin Nawfal (rahimahullah) aliposikia sifa hizi kubwa za Abdullah bin Masood (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwa Muaaz bin Jabal (Radhiyallahu ‘anhu), alishangaa. Alisema, “Nilifikiri mimi mwenyewe kwamba pengine Abdullah bin Masoud (Radhiya Allaahu anhu) amekosea (katika kauli yake wakati wa kumsifu Mu’aaz (Radhiya Allaahu ‘anhu)), kwa sababu sifa hizo zinapatikana ndani ya Quraan Majeed kwa Ibrahim (‘alayhis salaam). Ndani ya Quran Majeed, Allah Ta’ala amemsifu Ibrahim (alayhis salam) akisema:
إن إبراهيم كان أمة قانتا لله حنيفا
Pengine, Abdullah bin Masoud (Radhiya Allaahu ‘anhu) aliona mshangao wa Farwah bin Nawfal, hivyo akamtajia, “Je, unajua “Ummah” na “Qaanit” zinarejelea nini (kama ilivyotajwa pia katika kumsifu Nabi Ibrahim (alayhis salam) ndani ya Quraan Majeed?” Nikamjibu, “Mwenyezi Mungu ndiye anajua zaidi.”
Kisha Abdullah bin Masuud (Radhiya Allaahu ‘anhu) akaniambia: “Ummah inahusu mtu anayewafundisha watu wema (na kuwaongoza kwenye dini); na Qaanit inahusu mtu ambaye ni mtiifu kwa Allah Ta’ala na Mtume Wake (Sallallahu alaihi wasallam) wakati wote. Sifa hizi zilipatikana kwa Muaaz bin Jabal. Siku zote alionekana kuwafundisha watu dini, wakati yeye pia alibaki mtiifu kila wakati mnyenyekevu kwa Allah Ta’ala na Mtume wake (Sallallahu alaihi wasallam).
Akisema maneno haya, Abdullah bin Masoud (Radhiya Allaahu ‘anhu) alimueleza Farwah bin Nawfal kwamba Muaaz bin Jabal (Radhiya Allaahu anhu) anafanana na Nabi Ibrahim (‘Alayhis Salaam) katika sifa hizi mbili nzuri, na hivyo pia alistahiki kusifiwa kwa kuwa na sifa hizi mbili ndani ya maisha yake.
Alislaam Juhudi za Kuleta uislam ndani ya maisha yetu