Ndani ya Quran Majeed, Siku ya Qiyaamah imetajwa na majina mbalimbali. Baadhi ya majina hayo ni “Siku ya Malipo”, “Siku ya Kukusanywa”, “Siku ya Hasara na Faida” (yaani hasara kwa makafiri na faida kwa waumini), na “Siku ya Mkutano” (yaani kukutana na Allah Ta‘ala).
Tunapochunguza majina haya, tunaelewa kwamba kila jina linaonyesha hali siku ya Qiyaamah itakuwepo.
Miongoni mwa majina ya Siku ya Qiyaamah pia ni “Siku ya Majuto.” Siku hii itakuwa ni siku ya majuto makubwa kwa makafiri, kama jinsi Allah Ta’ala Anavyoeleza katika Quraan Majeed:
(Ewe Muhammad !) Waonye (makafiri) kuhusu Siku ya Majuto, itakapopitishwa uamuzi (yaani waingizwe katika Moto wa Jahannam na wakae humo milele).
Kutokana na hili, tunaelewa kwamba Siku ya Qiyaamah itakuwa ni siku ya majuto yasiyofikirika kwa makafiri.
Hata hivyo, kama vile itakavyokuwa siku ya majuto makubwa kwa makafiri, pia itakuwa, kwa kiasi fulani, siku ya majuto kwa baadhi ya waumini.
Majuto Pekee ya Watu wa Jannah
Kuhusiana na majuto ya Waumini, Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: “(Kabla ya kuingia Jannah), majuto pekee ambayo watu wa Jannah watakuwa nayo ni nyakati zilizopita (duniani) bila ya wao kumdhukuru Allah Ta’ala.”
Wakati Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) Atakapokuwa akiwapa waja Wake malipo makubwa na adhimu kwa muda walioutumia katika kumkumbuka, waumini wengine watajawa na huzuni na majuto juu ya muda na fursa zenye thamani walizozipoteza duniani bila kumdhukuru Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala).
Alislaam Juhudi za Kuleta uislam ndani ya maisha yetu