Fudhail bin Iyaaz (Rahimahullah) alikuwa Muhaddith mashuhuri na mchamungu mkubwa wa zama zake.
Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) alimbariki na daraja la juu katika Hadith kiasi kwamba Muhadditheen mashuhuri wengi, kama Abdullah bin Mubaarak, Sufyaan bin Uyainah na Imaam Shaafi’i (Rahimahumullah) wamesimulia Hadith kutoka kwake.
Imeripotiwa kwamba kabla ya Fudhail (rahimahullah) kubarikiwa na daraja la juu la uchamungu, alijulikana kuwa ni jambazi mashuhuri barabarani. Lakini, Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) akajalia tawfiq ya kutubia dhambi zake na kurekebisha maisha yake.
Alislaam Juhudi za Kuleta uislam ndani ya maisha yetu