Dua Na Adhkaar Kabla Ya Kulala 4

Dua Ya kumi

لَا إِلٰهَ إِلَّا اللهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيْكَ لَهُ لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ وَهُوَ عَلٰى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيْرٌ وَلَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللهِ سُبْحَانَ اللهِ وَبِحَمْدِهِ لَا إِلٰهَ إِلَّا اللهُ وَاللهُ أَكْبَرُ

Hakuna mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Allah Ta’ala Peke Yake. Hana mshirika. Kwake yeye ni ufalme wote, na sifa njema zote ni zake, na Yeye ndiye Mwenye uweza wa kila kitu, na hakuna uwezo (wa kujiepusha na madhambi) na hakuna nguvu (ya kuyatenda matendo mema) isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala). Ametakasika Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) kwa sifa zake! Hakuna mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Allah, na Allah Ta’ala ndiye Mkubwa zaidi.

Kumbuka: Kupitia kusoma dua hii kabla ya kulala, madhambi yote ndogo ndogo yatasamehewa, hata kama ni nyingi zaidi kuliko povu la bahari.

Dua Ya Kumi na Moja

اَللّٰهُمَّ اغْفِرْ لِيْ وَاخْسَأْ شَيْطَانِيْ وَفُكَّ رِهَانِيْ وَثَقِّلْ مِيْزَانِيْ وَاجْعَلْنِيْ فِيْ النَّدِيِّ الْأَعْلٰى

Ewe Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala)! Nisamehe madhambi zangu, na niepushe na Shet’ani wangu (asinidhuru), na uniweke huru (na minyororo za madhambi), na ufanye mizani yangu (ya matendo mema) kuwa nzito (Siku ya Qiyaamah), na nisababishie kuwa miongoni mwa mkusanyiko wa waja wako wema na Malaika.

About admin

Check Also

Dua Unapo Ota Ndoto Mbaya

Ikiwa unahofu usiku kwa sababu ya kuona ndoto mbaya, basi soma dua zifuatazo:

Dua Ya Kwanza

Naomba kujikinga na maneno kamili ya Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’alah), ambayo mchamungu wala muovu hawezi kuyapita; najikinga na shari yoyote inayoteremka kutoka mbinguni na inayopanda kwenda mbinguni, na najikinga na shari yoyote alichokiumba duniani na kinachotokea humo, na najikinga na mitihani za usiku na mitihani za mchana, na shari za viumbe wanaotoka usiku na mchana, isipokuwa wale wanaokuja kwa kheri, Ewe Mwingi wa Rehma.