Mchamungu wa Wakati Wake – Bishr Haafi (rahimahullah)

Bishr Haafi (rahimahullah) alikuwa mchamungu mashuhuri katika zama zake. Wakati mmoja, mtu fulani alimuuliza, “Umeipataje nafasi hii ya juu ya uchamungu na uadilifu tunayoiona?” Katika kujibu, Bishr (rahimahullah) alitaja yafuatayo:

Chochote ambacho nimebarikiwa nacho ni kupitia neema ya Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala). Hali yangu ya awali ilikuwa kwamba sikuwa mtu wa kujitolea kwa deen.

Siku moja, nilipokuwa nikitembea, niliona kipande cha karatasi chini. Pindi nilipoiokota, nikakuta jina la Allah Ta’ala limeandikwa juu yake. Niliinua macho yangu mbinguni na kusema, “Ewe Mwenyezi Mungu! Hili ni jina lako lililobarikiwa ambalo limetupwa chini!”

Kisha nilisafisha karatasi na kuiweka mfukoni mwangu kwa heshima zote.

Wakati huo, nilikuwa na dirham mbili tu. Nikaelekea kwenye duka la manukato, nikanunua manukato na kuipaka kwenye karatasi ile. Baada ya hapo, nilienda nyumbani, na kuiweka juu ya kabati.

Usiku ule, niliota ndoto ambayo ndani yake niliambiwa, “Ewe Bishr! Umeinuwa jina letu basi sisi tutainuwa jina lako duniani na akhera.” Ilikuwa ni kwa ajili ya kitendo hiki ambapo Mwenyezi Mungu alinipa nafasi hii.

Kutokana na tukio hili, tunaelewa kwamba wakati Bishr Haafi (rahimahullah) alionesha heshima kwenye jina la Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala), basi Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’alah) akambariki tawfeeq ya kubadilisha maisha yake.

Mbali na hayo, Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) Akambariki na ufahamu wa kweli wa Quran na Hadithi za Mtume (Sallallahu alaihi wasallam). Kwa hiyo, alihesabiwa miongoni mwa Muhaddithin wa zama zake.

Huo ndio ulikuwa msimamo wake mkubwa hadi Imaam mkubwa wa zama zake Imam Ahmad bin Hanbal (rahimahullah) amesimulia Hadithi kutoka kwake na kufaidika na ujuzi wake wa kina.

Maulamaa wanaeleza kuwa kuonyesha heshima kwa kitu chochote kile inayohusishwa na Dini (yaani Quran Majeed, Hadith, Msikiti, Adhaan, Maulamaa (masheikhe) , Huffaaz (wenye kuhifadhi Quran, n.k.) ni njia ya kupata baraka kubwa na kukubaliwa na Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala).

About admin

Check Also

Kuwa Na Moyo Wa Kusamehe

Waa’il bin Hujr (Radhiyallahu anhu) alikuwa sahaabi maarufu wa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) ambaye alitoka …