عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ ﴿١﴾ أَن جَاءَهُ الْأَعْمَىٰ ﴿٢﴾ وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُ يَزَّكَّىٰ ﴿٣﴾ أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ الذِّكْرَىٰ ﴿٤﴾ أَمَّا مَنِ اسْتَغْنَىٰ ﴿٥﴾ فَأَنتَ لَهُ تَصَدَّىٰ ﴿٦﴾ وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ ﴿٧﴾ وَأَمَّا مَن جَاءَكَ يَسْعَىٰ ﴿٨﴾ وَهُوَ يَخْشَىٰ ﴿٩﴾ فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ ﴿١٠﴾ كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ ﴿١١﴾ فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ ﴿١٢﴾ فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ ﴿١٣﴾ مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ ﴿١٤﴾
Yeye (Mtume [Sallallahu alaihi wasallam]) alikunja uso na akageuka kwa sababu yule kipofu alimjia! Na nini kitakujulisha (Ewe Muhammad [Sallallahu alaihi wasallam] kuhusu hali ya huyo kipofu?) Pengine, (kama ungemhudumia), angeweza kupata utakaso, au angepata ushauri, na ushauri ungemfaa. Ama yule ambaye hajali (kuhusu Imaan na Dini), basi wewe unamjali (zaidi), na wala si lawama juu yako ikiwa hakupata utakaso. (Lakini) ama aliyekujia kwa juhudi, na hali ya kuwa anahofu na (Allah Ta‘ala na kuwajibika Akhera), basi wewe unajiepusha naye! Kamwe! (Usifanye hivyo!) Hakika (Qur-aan Majeed) ni ukumbusho (na mawaidha). Basi anayetaka basi atazingatia. (Qur-aan Majeed) (imeandikwa) katika karatasi za heshima, imetukuka zaidi, (na) imetakasika, (imeandikwa) na mikono ya wale waandishi (Malaika wanaoiandika kutoka Lowh-ul-Mahfuudh, Malaika ambao) watukufu (na) wema.
Wakati mmoja, Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alikuwa akijadiliana na baadhi ya viongozi wa Maquraish, akiwalingania kwenye Uislamu. Miongoni mwa viongozi hao walikuwa ni Utbah bin Rabi’ah, Abu Jahl bin Hishaam, na ami yake mheshimiwa Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhu), ambao hadi wakati huo walikuwa bado hawajasilimu.
Wakati wa majadiliano hayo, Abdullah bin Ummi Maktoom (Radhiyallahu ‘anhu), Sahaabi kipofu wa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam), alifika na kuanza kumuuliza Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) baadhi ya maswali yanayohusiana na dini.
Katika riwaya iliyonukuliwa na Allaamah Baghawi (Rahimahullah), imetajwa kuwa kwa sababu Abdullah bin Ummi Maktoom (Radhiya Allaahu ‘anhu) alikuwa kipofu, hakutambua kuwa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alikuwa akijadiliana na viongozi wa Maquraish. Kwa hiyo, alipoingia kwenye mkusanyiko, hapo hapo aliuliza maswali yake na kukatiza mazungumzo.
Kwa mujibu wa Haafidh Ibn Kathir (rahimahullah), Ibnu Ummi Maktum (radhiyallahu ‘anhu) alitaka Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) amfundishe aya ya Qur-aan Majeed. Lakini, kwa vile Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alikuwa amejishughulisha na kuwakhutubia viongozi wa Maquraish na kuwalengania kwenye Dini, hakuwa makini na Sahaabi huyu bali aliendelea kuwahutubia viongozi wa Maquraishi.
Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alikataa kukatizwa kwa maswahaba, na dalili za kutoridhishwa kwake na kutoridhika kwake zilionekana kwenye uso wake.
Ilikuwa ni katika tukio hilo ambapo Allah Ta’ala aliteremsha aya kumi na nne za mwanzo za surah hii, ili kumsahihisha Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) na kutoa muongozo kwa ummah wake kuhusu jinsi mtu anavyopaswa kufanya na kutenda katika hali kama hiyo.
Alislaam Juhudi za Kuleta uislam ndani ya maisha yetu