Tafseer Ya Surah Abas

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ ‎﴿١﴾‏ أَن جَاءَهُ الْأَعْمَىٰ ‎﴿٢﴾‏ وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُ يَزَّكَّىٰ ‎﴿٣﴾‏ أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ الذِّكْرَىٰ ‎﴿٤﴾‏ أَمَّا مَنِ اسْتَغْنَىٰ ‎﴿٥﴾‏ فَأَنتَ لَهُ تَصَدَّىٰ ‎﴿٦﴾‏ وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ ‎﴿٧﴾‏ وَأَمَّا مَن جَاءَكَ يَسْعَىٰ ‎﴿٨﴾‏ وَهُوَ يَخْشَىٰ ‎﴿٩﴾‏ فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ ‎﴿١٠﴾‏ كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ ‎﴿١١﴾‏ فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ ‎﴿١٢﴾‏ فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ ‎﴿١٣﴾‏ مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ ‎﴿١٤﴾‏

Yeye (Mtume [Sallallahu alaihi wasallam]) alikunja uso na akageuka kwa sababu yule kipofu alimjia! Na nini kitakujulisha (Ewe Muhammad [Sallallahu alaihi wasallam] kuhusu hali ya huyo kipofu?) Pengine, (kama ungemhudumia), angeweza kupata utakaso, au angepata ushauri, na ushauri ungemfaa. Ama yule ambaye hajali (kuhusu Imaan na Dini), basi wewe unamjali (zaidi), na wala si lawama juu yako ikiwa hakupata utakaso. (Lakini) ama aliyekujia kwa juhudi, na hali ya kuwa anahofu na (Allah Ta‘ala na kuwajibika Akhera), basi wewe unajiepusha naye! Kamwe! (Usifanye hivyo!) Hakika (Qur-aan Majeed) ni ukumbusho (na mawaidha). Basi anayetaka basi atazingatia. (Qur-aan Majeed) (imeandikwa) katika karatasi za heshima, imetukuka zaidi, (na) imetakasika, (imeandikwa) na mikono ya wale waandishi (Malaika wanaoiandika kutoka Lowh-ul-Mahfuudh, Malaika ambao) watukufu (na) wema.

About admin

Check Also

Tafseer Ya Surah Falaq Na Surah Naas

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ ‎﴿١﴾‏ مِن شَرِّ مَا خَلَقَ ‎﴿٢﴾‏ وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ ‎﴿٣﴾‏ وَمِن …