Tafseer Ya Surah Naazi’aat

وَالنَّازِعَاتِ غَرْقًا ‎﴿١﴾‏ وَالنَّاشِطَاتِ نَشْطًا ‎﴿٢﴾‏ وَالسَّابِحَاتِ سَبْحًا ‎﴿٣﴾‏ فَالسَّابِقَاتِ سَبْقًا ‎﴿٤﴾‏ فَالْمُدَبِّرَاتِ أَمْرًا ‎﴿٥﴾

Ninaapa kwa wale (malaika) ambao wanao toa (roho za makafiri) kwa nguvu, na kwa wale (malaika) wanao toa (roho za waumini) kwa upole, na kwa wale (malaika) ambao wanapaa (angani) kwa haraka, na kwa wale (malaika) ambao wanashindana mbio (kutimiza amri za Allah Ta’ala), na wale (malaika) ambao wanasimamia mambo (wameamriwa kutimiza na Mwenyezi Mungu subhaanahu wata’ala,)

Kama vile Surah iliopita – Surah Naba – iliteremshwa kuthibiti imani ya siku ya Qiyamaah, hivyo Surah hii pia iliteremshwa kujadili mambo kadhaa ya Qiyaamah.

Katika Surah hii, Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) anaanza na kuchukua viapo juu ya sifa fulani za malaika ili kudhibitisha kwamba siku ya Qiyaamah ni hakika. Kwa hivyo, katika aya ya sita, baada ya kuchukua kiapo juu ya sifa za malaika, Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) anasema juu ya siku ya Qiyaamah.

Sababu dhahiri ya Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) kuchukua viapo kwa malaika ambao huondoa roho za watu ni kumjulisha mwanadamu kwamba kila mtu qiyaamah yake itaanza baada ya kufariki. Kwa hivyo, inasemekana, “Yule anayefariki, Qiyaamah yake inaanza.”

Ingawa Qiyaamah halisi kwa viumbe wote itafanyika mwishoni mwa ulimwengu, hata hivyo kwa kuwa maisha ya aakhera ya kila mtu itaanza wakati wa kifo chake, kifo cha kila mtu kinahesabiwa kuwa Qiyaamah yake.

Kwa jumla, katika aya hizi, Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) anaangazia sifa tano za malaika. Sifa tano ni hizi zifuatavyo:

Sifa ya kwanza ya malaika

وَالنَّازِعَاتِ غَرْقًا ‎﴿١﴾‏

Ninaapa kwa wale (malaika) ambao hutoa (roho za makafiri) kwa nguvu

Katika aya hii, Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) anaongea juu ya malaika wa kifo ambao hutoa roho za makafiri kwa nguvu na kwa ukali, kwa nguvu kamili, bila kuwaonyesha huruma yoyote. Malaika ambao huondoa roho za makafiri ni malaika wa adhabu, na neno “kwa nguvu” katika aayah linamaanisha maumivu ya kiroho, sio maumivu ya mwili. Kwa hivyo, watu ambao wapo karibu na mtu anayekufa hawawezi kuona maumivu ya mtu anayekufa kwa sababu maumivu yanahisi na roho ya mtu anayekufa, na sio mwili wake.

Wakati mwingine, inaonekana ingawa roho ya kafiri inatoka kwenye mwili wake kwa urahisi, lakini kwa ukweli sio hivyo, kama ilivyo katika aya hii, Allah Ta’ala anatuarifu juu ya uchungu mkubwa na mateso ambayo roho ya kafiri hupitia wakati wa kifo.

About admin

Check Also

Tafseer Ya Surah Ikhlaas

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ ‎﴿١﴾‏ اللَّهُ الصَّمَدُ ‎﴿٢﴾‏ لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ ‎﴿٣﴾‏ وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا …