Uhusiano Wa Karibu Kati Ya Abdullah bin Mas’uud (radhiyallahu ‘anhu) na Mtume (Sallallahu alaihi wasallam)

Abu Muusa Ash’ari (Radhiya Allaahu ‘anhu) anaeleza, “Mimi na kaka yangu tulipokuja kutoka Yemen (kuja Madinah Munawwarah), basi kwa muda fulani tulifikiri kwamba Abdullah bin Mas’uud (Radhiya Allaahu ‘anhu) na mama yake ni miongoni ya watu ambao wanaishi nyumbani kwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) kwa sababu ya wao kuingia mara kwa mara nyumbani kwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) na pia uhusiano wao wa karibu naye.” (Sahih Bukhari #4384)

About admin

Check Also

Kufariki Kwa Abu Dhar (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Wakati Abu Dhar (Radhiya Allaahu ‘anhu) alipokaribia mwisho wake, hapakuwa na mtu yoyote pamoja naye …