Sunna Za Msikiti.

13. Usipaze sauti yako au kufanya kelele ndani ya msikiti na katika eneo linalozunguka musjid.[1]

عن السائب بن يزيد رضي الله عنه قال كنت نائما في المسجد فحصبني رجل فنظرت فإذا عمر بن الخطاب رضي الله عنه فقال اذهب فأتني بهذين فجئته بهما فقال ممن أنتما أو من أين أنتما قالا من أهل الطائف قال لو كنتما من أهل المدينة لأوجعتكما ترفعان أصواتكما في مسجد رسول الله صلى الله عليه وسلم (صحيح البخاري، الرقم: 470)[2]

Sayyiduna Saaib bin Yazid (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba, “Wakati mmoja, nilikuwa nimelala msikitini wakati mtu fulani alinirushia kokoto (ili kuniamsha). Nilitazama na nikaona kwamba alikuwa ni Umar (radhiyallahu ‘anhu) Akaniambia, ‘Nenda uniletee watu hawa wawili kwangu.’ Nikawaleta mbele yake, na akawauliza, ‘Nyinyi watu wawili mnatoka wapi?’ Wakajibu kwamba wao wanatoka Taaif. Sayyidina Umar (radhiyallahu ‘anhu) akasema, ‘Lau ungekuwa katika watu wa Madinah Munawwarah, mimi ningewadhibuni! mnapaza sauti zenu katika msikiti wa Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam)!’

عن أبي هريرة رضي الله عنه قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم إذا اتخذ الفيء دولا والأمانة مغنما والزكاة مغرما وتعلم لغير الدين وأطاع الرجل امرأته وعق أمه وأدنى صديقه وأقصى أباه وظهرت الأصوات في المساجد وساد القبيلة فاسقهم وكان زعيم القوم أرذلهم وأكرم الرجل مخافة شره وظهرت القينات والمعازف وشربت الخمور ولعن آخر هذه الأمة أولها فارتقبوا عند ذلك ريحا حمراء وزلزلة وخسفا ومسخا وقذفا وآيات تتابع كنظام قطع سلكه فتتابع (سنن الترمذي، الرقم: 2211)[3]

Sayyidina Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba Sayyidina Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Wakati ngawira za vita zitachukuliwa kama mali ya watu ili kugawanywa miongoni mwao, wakati amana itachukuliwa kuwa ni ngawira (yaani mali ya umma), wakati zakaah itachukuliwa kuwa ni ushuru, wakati elimu ya Dini itakapopatikana kwa nia zisizokuwa za dini, pindi mwanamume atakapomtii mkewe na kumuasi mama yake, na kumweka rafiki yake karibu naye na kumtenga baba yake mzazi na sauti zitapazwa msikitini, na mkosaji wa kabila moja atakuwa kiongozi wao, na mtu wa chini kabisa atakuwa mwakilishi wao, na mtu ataheshimiwa kwa kuogopa uovu wake, na waschana wa kuimba na vyombo vya mziki vitaongezeka, na pombe itanywewa (hadharani), Na watu wa mwisho wa Ummah huu watawalaani watu wa kabla yao Katika umma huu, (zitakapodhihiri dalili hizi) basi watu wangoje vimbunga, matetemeko ya ardhi, watu kuzama ardhini, kuharibika kwa uso, mawe yanayonyesha kutoka mbinguni na mengine yanayofanana na hayo zitakazofuatana mmoja baada ya nyingine, kama vile lulu katika uzi huanguka kwa kufuatana wakati uzi unapokatwa.


[1] تكره الخصومة في المسجد ورفع الصوت فيه ونشد الضالة وكذا البيع والشراء والاجارة ونحوها من العقود هذا هو الصحيح المشهور (المجموع شرح المهذب 2/141)

[2] قال الحافظ في الفتح (1/656): قوله كنت قائما في المسجد كذا في الأصول بالقاف وفي رواية نائما بالنون ويؤيده رواية حاتم عن الجعيد بلفظ كنت مضطجعا

[3] قال أبو عيسى: وفي الباب عن علي وهذا حديث غريب

وعن علي رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال إذا فعلت أمتي خمس عشرة خصلة فقد حل بها البلاء قيل وما هي يا رسول الله قال إذا كان المغنم دولا وإذا كانت الأمانة مغنما والزكاة مغرما وأطاع الرجل زوجته وعق أمه وبر صديقه وجفا أباه وارتفعت الأصوات في المساجد وكان زعيم القوم أرذلهم وأكرم الرجل مخافة شره وشربت الخمر ولبس الحرير واتخذت القينات والمعازف ولعن آخر هذه الأمة أولها فليرتقبوا عند ذلك ريحا حمراء أو خسفا أو مسخا رواه الترمذي وقال لا نعلم أحدا روى هذا الحديث عن يحيى بن سعيد الأنصاري غير الفرج بن فضالة (سنن الترمذي، الرقم: 2210)

About admin

Check Also

Sunna Za Msikiti

27. Uwe mtulivu na mwenye heshima ukiwa msikitini, wala usighafilike na kusahau heshima ya msikiti. …