Sifa za Muadhini

1. Muadhin anatakiwa awe mwanamume.[1]

عن ابن عمر رضي الله عنهما قال ليس على النساء أذان ولا إقامة (السنن الكبرى للبيهقي، الرقم: 1996)[2]

Imepokelewa kwamba Sayyidina Ibnu Umar (radhiyallahu ‘anhu) amesema, “kutowa adhana na iqaamah si jukumu la mwanamke.

2. Awe na akili timamu.[3]

3. Awe na umri wa kuelewa. Adhaan ya mtoto mdogo ambaye hajafikia umri wa kuelewa si sahihi[4]

4. Awe na uwezo wa kutamka maneno ya adhana kwa usahihi.

5. Awe na elimu ya nyakati za swalah.[5]

6. Awe Muislamu mchamungu na muislamu alie nyooka.[6]

عن ابن عباس رضي الله عنهما قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم ليؤذن لكم خياركم وليؤمكم قراؤكم (سنن أبي داود، الرقم: 590)[7]

Sayyidina Ibnu Abbas (radhiyallahu ‘anhuma) anaripoti kwamba Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) amesema: “Yule bora zaidi miongoni mwenu (mchamungu zaidi) achaguliwe kutoa adhana, na qari bora miongoni mwenu (yaani mwenye elimu zaidi katika kusoma na masaail za swalah) awaongoze katika swalah.”

Maelezo: Sifa tatu za mwanzo zilizotajwa ni masharti ya uhalali wa adhana. Kwa hivyo ikiwa hazitapatikana, adhana haitakuwa sahihi.


[1] فصل في صفة المؤذن وآدابه وشرطه أن يكون … ذكرا (روضة الطالبين 1/312)

[2] لهذا الحديث شاهد مرسل من حديث إبراهيم النخعي: حدثنا محمد بن الحسن الشيباني قال أخبرنا أبو حنيفة عن حماد عن إبراهيم قال ليس على النساء أذان ولا إقامة (كتاب الآثار، الرقم: 64)

[3] فصل في صفة المؤذن وآدابه وشرطه أن يكون … عاقلا (روضة الطالبين 1/312)

[4] (و) شرط من ذكر (التمييز) فلا يصحان من غير مميز لعدم أهليته للعبادة (مغني المحتاج 1/323)

[5] استحب كونه عالما بالمواقيت (مغني المحتاج 1/333)

[6] فصل في صفة المؤذن وآدابه … ويستحب … أن يكون عدلا وهو الثقة (روضة الطالبين 1/312-313)

[7] سكت الحافظ عن هذا الحديث في الفصل الثاني من هداية الرواة (2/4) فالحديث حسن عنده

About admin

Check Also

Chanzo cha nuru siku ya Qiyaama

عن ابن عمر رضي الله عنهما قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم زينوا …