Mfumo wa Allah Ta‘ala, kuhusiana na jinsi mwanadamu alivyo umbwa, ni kwamba wakati mambo mawili yanapopatikana basi mwanadamu atapatikana. Sababu ya kwanza ni njia ya wazazi ambayo mbegu ya mwanaume hupandwa ndani ya tumbo la mama. Sababu ya pili ni roho kupulizwa ndani ya tumbo baada ya kukamilisha miezi minne.
Kila mtu aliyekuja duniani alifuata mfumo huu. Lakini, Allah Ta’ala amewafanya watu watatu kuwa tofauti na kanuni hii yaani Nabii Aadam, Hawwaa, na Nabii Isa (‘alaihimus salaam).
Kuhusiana na Nabii Aadam (‘alayhis salaam), Allah Ta’ala aliutengeneza umbo lake na mchanga na kisha akapuliza rooh ndani yake. Kwa hivyo, alizaliwa bila njia ya wazazi wawili.
Ama Hawwaa (‘Alaihas salaam), Allah Ta‘ala alimuumba kutoka ubavu wa kushoto wa Nabi Aadam (‘alayhis salaam). Kwa hivyo, alizaliwa kupitia njia ya mwanamume tu.
Ama Nabii Isa (‘alaihis salaam), basi Allah Ta’ala alimuumba kwa kupuliza roho ndani ya tumbo la mama yake. Kwa hiyo, alizaliwa kupitia njia ya mwanamke pekee.
Katika Qur-aan Majeed, Nabii Isa (‘alayhis salaam) amefananishwa na Aadam (‘alayhis salaam). Allah Ta’ala Anasema:
Hakika mfano wa Nabii Isa (‘alayhis salaam) kwa Mwenyezi Mungu ni sawa na mfano wa Nabii Aadam (‘alayhis salaam). Allah Ta’ala alimuumba (Nabii Aadam) na mchanga, kisha akauambia (mchanga): “Kuwa! naye akatokea.” (Sura Aal–Imraan aya ya 59)
Katika Aaya hii, Allah Ta‘ala anaeleza kwamba uumbaji wa Nabii Isa (‘alaihis salaam) ulifanana na uumbaji wa Nabii Aadam (‘alaihis salaam) kwa maana ya kwamba Nabii Aadam (‘alayhis salaam) hakuzaliwa kupitia njia ya wazazi, bali aliumbwa na ruhu kupulizwa ndani yake.
Vile vile, Nabii Isa (‘alayhis salaam) hakuzaliwa kupitia njia ya baba, kwa sababu Ruhu ulipulizwa tumboni mwa mama yake, na kusababisha yeye kuwepo.
Kwa hivyo, tunaona kwamba kama jinsi uumbaji wa Nabi Aadam (‘alayhis salaam) na Hawwaa (‘alaihas salaam) ulivyotokea na mujiza, hivyo hivyo uumbaji wa Nabii Isa (‘alayhis salaam) ulikuwa wa kimujiza.
Alislaam Juhudi za Kuleta uislam ndani ya maisha yetu