Isa (‘alayhis salaam) ni Mtume wa Allah Ta‘ala na anahesabiwa miongoni mwa manabii wa daraja la juu. Allah Ta’ala alimteremshia Injili (Biblia) na akamjalia na Shari’ah. Yeye ndiye Nabii aliyetumwa duniani kabla ya Mtume (Sallallahu alaihi wasallam).
Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) amesema: “Manabii wote ni kama ndugu wa baba mmoja, mama zao wanatofautiana, na Dini yao ni moja (yaani wote wanaamini tauheed – umoja wa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala), ingawa Shari’ah zao ni tofauti). Mimi ndiye mtu wa karibu sana wa Nabii Isa bin Maryam (‘alayhis salaam), kwa sababu hakuna Nabii baina yetu. Hakika Nabii Isa (‘alayhis salaam) atashuka.” (Musnad Ahmed #9270)
Allah Ta’ala alimtuma Nabii Isa (‘Alayhis Salaam) kwa Bani Israa’il, lakini hawakumuamini na wakamkataa. Walijaribu hata kumuua, lakini Allah Ta’ala akamlinda na akamnyanyua mbinguni akiwa hai. Hivi sasa, Nabii Isa (‘Alayhis Salaam) yupo hai mbinguni, na kabla ya Qiyaamah, Allah Ta’ala atamrudisha duniani.
Katika Hadith, Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) amesema, “Naapa kwa Yule ambaye maisha yangu yapo mkononi mwake! Nabii Isa (‘alayhis salaam)) atashuka kutoka mbinguni, na atatawala miongoni mwenu kama mtawala mwadilifu. Atauvunja msalaba na kuua nguruwe…” (Sahih Muslim #155)
Alislaam Juhudi za Kuleta uislam ndani ya maisha yetu