Dua baada ya Adhaan

1. Baada ya adhaan, mtu anatakiwa amswalie nabi wa Allah (sallallahu ‘alaihi wasallam) na baada ya hapo asome dua ifuatayo:[1]

اَللّٰهُمَّ رَبَّ هٰذِهِ الدَّعْوَةِ التَّامَّةِ وَالصَّلَاةِ الْقَائِمَةِ آتِ مُحَمَّدًانِ الْوَسِيْلَةَ وَالْفَضِيْلَةَ وَابْعَثْهُ مَقَامًا مَّحْمُوْدًانِ الَّذِيْ وَعَدْتَّهُ إِنَّكَ لَاتُخْلِفُ الْمِيْعَادْ

Ewe Allah, Mola wa wito huu mkamilifu na ulio thibiti Swalaah, mpe Sayyidina Muhammad (sallallahu ‘alaihi wasallam)‘waseelah’ (hatua ya juu sana katika Jannah) na ‘fadheelah’ (nafasi ya juu iliyo juu ya uumbaji wote), na umjalie “Maqaam Mahmood” (yaani heshima ya uombezi kwa Allah kuanza hesabu wa viumbe vyote Siku ya Qiyaamah) uliyomuahidi, hakika Wewe uwendi kinyume na ahadi yako.

عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما أنه سمع النبي صلى الله عليه وسلم يقول إذا سمعتم المؤذن فقولوا مثل ما يقول ثم صلوا علي فإنه من صلى علي صلاة صلى الله عليه بها عشرا ثم سلوا الله لي الوسيلة فإنها منزلة في الجنة لا تنبغي إلا لعبد من عباد الله وأرجو أن أكون أنا هو فمن سأل لي الوسيلة حلت له الشفاعة (صحيح مسلم، الرقم: 384)

Sayyiduna Abdullah bin Amr bin Aas (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba alimsikia Sayyidina Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) akisema, “Mnapomsikia muadhin akitoa Adhaan, rudia maneno ya adhaan baada yake na baada ya hapo niswalie (kabla kusoma dua ya adhaan). Hakika mwenye kuniswalia juu yangu mara moja, Allah humteremshia baraka kumi. Kisha (soma dua baada ya adhana ambayo ndani yake) muombe Allah kunibariki kwa heshima ya ‘waseelah’ ambayo ni nafasi ya juu na daraja katika Jannah ambayo itawekewa kwa mmoja wa waja wa Allah Ninatumai kwa dhati kuwa nitapewa nafasi hiyo, na anayeomba dua kwa Allah ku nipa ‘waseelah’, atapata uombezi wangu siku hiyo ya Qiyaamah.”

عن جابر رضي الله عنه قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم من قال حين يسمع النداء اللهم رب هذه الدعوة التامة والصلاة القائمة آت محمدا الوسيلة والفضيلة وابعثه مقاما محمودا الذي وعدته حلت له شفاعتي يوم القيامة (صحيح البخاري، الرقم: 614) (وأما زيادة إنك لا تخلف الميعاد فقد ذكرها البيهقي في السنن الكبرى، 1/410)

Sayyiduna Jaabir (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba Sayyidina Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) kasema: “Mwenye kusoma dua ifuatayo baada ya adhaan, atapata uombezi wangu siku ya Qiyaamah.”

اَللّٰهُمَّ رَبَّ هٰذِهِ الدَّعْوَةِ التَّامَّةِ وَالصَّلَاةِ الْقَائِمَةِ آتِ مُحَمَّدًانِ الْوَسِيْلَةَ وَالْفَضِيلَةَ وَابْعَثْهُ مَقَامًا مَّحْمُودًانِ الَّذِيْ وَعَدْتَّهُ (إِنَّكَ لَاتُخْلِفُ الْمِيْعَادْ)


[1] ثم يصلي على النبي صلى الله عليه وسلم … ثم يسأل الله تعالى الوسيلة فيقول اللهم رب هذه الدعوة التامة والصلاة القائمة آت سيدنا محمدا الوسيلة والفضيلة وابعثه مقاما محمودا الذي وعدته … أما أحكام الفصل فقال أصحابنا يستحب للمؤذن أن يقول بعد فراغ أذانه هذه الأذكار المذكورة من الصلاة على رسول الله صلى الله عليه وسلم وسؤال الوسيلة (المجموع شرح المهذب 3/86-87)

About admin

Check Also

Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu …