Aina Za Sunna Za Kufanya Istinja – Saheemu Ya Tano

17. Chukuwa tahadhari sana kuhakikisha kuwa hupatwi na cheche za mkojo mwilini. Hukifanya uzembe kwa hili kuna adhabu kaburini.[1]

عن أبي هريرة رضي الله عنه قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم أكثر عذاب القبر من البول (سنن ابن ماجة، الرقم: ٣٤٨)[2]

Sayyidina Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) alisema kuwa mtume (sallallahu ‘alaihi wassallam) amesema ” adhabu kali (zitakazo wakabili watu wengi) kaburini ni adhabu za mkojo (mf: mtu kutokuwa makini kwa cheche za mkojo ambazo zinampata. Kwa ajili ya hilo udhu, sala zao na ibada zingine hazitokubalika kwa kuwa mtu anakuwa mchafu”)

18. Wakati hukifanya istinja tumia mawe ya udongo au ( tishu za chooni) kisha tumia maji kwa kujisafisha, uhakikishe umejaza maji kwenye kopo kabla ujajisaidia unaweza ukajiweka kwenye shida hukikuta hakuna maji.[3]

عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال نزلت هذه الآية في أهل قباء فيه رجال يحبون أن يتطهروا قال كانوا يستنجون بالماء فنزلت فيهم هذه الآية (سنن الترمذي، الرقم: ٣١٠٠)[4]

Sayyidina Abu Hurairah(radhiyallahu ‘anhu) alitowa ripoti kuwa mtume (sallallahu ‘alaihi wassallam) amesema “aya hii فيه ر جال يحبون ان يتطهروا ( ndani mwake kuna wanaume ambao wanapenda kujisafisha) aya hii ilikuwa imeshuka kwa ajili ya watu wa qubaa kwakuwa walikuwa wanafanya istinja kwa kutumia maji.

قال علي رضي الله عنه إن من كان قبلكم كانوا يبعرون بعرا وإنكم تثلطون ثلطا فأتبعوا الحجارة بالماء (المصنف لابن أبي شيبة، الرقم: ١٦٤٥)

Sayyidina Ali (radhiyallahu ‘anhu) alisema haja kubwa za watu kabla ya nyinyi zilikuwa ngumu na kavu na haja kubwa zenu ni nyepesi sana (yaani ni kutokana na utofauti wa chakula) kwahiyo fanya istinja kwa kutumia mawe ya udongo baada ya hapo tumia maji kwa kujisafisha zaidi (yaani: kuondowa uchafu utakao kuwa umebaki kwenye sehemu za siri)

19. Tumia mkono wako wa kushoto kujisafisha. Kufanya istinja na mkono wa kulia ni makruu. Vile vile usishike sehemu zako za siri kwa mkono wa kulia.[5]

عن عبد الله بن أبي قتادة عن أبيه رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال إذا بال أحدكم فلا يأخذن ذكره بيمينه ولايستنجي بيمينه (صحيح البخاري، الرقم: ١٥٤)

Sayyidina Abdullah Bin Abi Qataadah (radhiyallahu ‘anhu) amesema kutoka kwa baba yake kuwa mtume (sallallahu ‘alaihi wassallam) amesema “kati yenu mmoja wenu akiwa anajisaidia asishike sehemu za siri kutumia mkono wa kulia na wala usifanye istinja kwa mkono wa kulia.”


[1] ومنها ان لا يبول في مهاب الرياح استنزاها من البول وحذارا من رشاشه  قال صلى الله عليه وسلم استنزهوا من البول فان عامة عذاب القبر منه (فتح العزيز ١/٤٦٦-٤٦٧)

[2] قال العلامة البوصيري: هذا إسناد صحيح رجاله عن آخرهم محتج بهم فى الصحيحين (زوائد ابن ماجة صـ ٨١)

[3] قال المصنف رحمه الله (واذا أراد الاستنجاء نظرت فان كانت النجاسة بولا أو غائطا ولم تجاوز الموضع المعتاد جاز بالماء والحجر والافضل أن يجمع بينهما … فان أراد الاقتصار على أحدهما فالماء أفضل لأنه ابلغ في الانقاء وان أراد الاقتصار على الحجر جاز …) … أما حكم المسألة فقال أصحابنا يجوز الاقتصار في الاستنجاء على الماء ويجوز الاقتصار على الأحجار والأفضل أن يجمع بينهما فيستعمل الأحجار ثم يستعمل الماء (المجموع شرح المهذب 2/81-83)

الأفضل أن يجمع في الاستنجاء بين الماء والجامد، ويقدم الجامد. فإن اقتصر، فالماء أفضل (روضة الطالبين 1/181)

[4] وأما حديث أبي هريرة رضي الله عنه فأخرجه أبو داود والترمذي وابن ماجه مرفوعا قال نزلت هذه الآية في أهل قباء فيه رجال يحبون أن يتطهروا والله يحب المطهرين قال كانوا يستنجون بالماء فنزلت فيهم هذه الآية وسنده ضعيف وفي الباب أحاديث صحيحة أخرى ومن هنا ظهر أن قول من قال من الأئمة إنه لم يصح في الاستنجاء بالماء حديث ليس بصحيح (تحفة الأحوذي 1/94)

[5] أما حكم المسألة فقال الأصحاب يكره الاستنجاء باليمين كراهة تنزيه ولا يحرم (المجموع شرح المهذب 2/88)

المستحب أن يستنجي باليسار (روضة الطالبين 1/181)

About admin

Check Also

Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu …