Sunna Za Msikitini

9. Fanya niya ya nafil i’tikaaf kwa ajili ya kuwa utakaa msikitini.[1]

10. Swali rakaa mbili za tahiyyatul masjid ukiingia msikitini.[2]

عن أبي قتادة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال إذا دخل أحدكم المسجد فليركع ركعتين قبل أن يجلس (صحيح البخاري، الرقم: 444)

Sayyidina Abu Qataadah (radhiyallahu ‘anhu) amesema kuwa Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam alisema, ” pindi mmoja wenu atakapo ingia msikitini, anatakiwa kuswali rakaa mbili za swala kabla ya kukaa,”

11. Usifanye shughuli ya biashara yoyote msikitini.[3]

عن عمرو بن شعيب عن أبيه عن جده رضي الله عنهما قال نهى رسول الله صلى الله عليه وسلم عن تناشد الأشعار في المسجد وعن البيع والاشتراء فيه وأن يتحلق الناس يوم الجمعة قبل الصلاة في المسجد (سنن الترمذي، الرقم: 322)[4]

Sayyidina Abdullah Bin Amr (radhiyallahu ‘anhuma)  ameripoti kuwa, “Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) amesema marufuku kuimba shairi katika Msikitini, kununua na kuuza katika msikiti, na watu kukaa makundi katika msikiti siku ya ijumaa kabla ya swala ya ijumaa ( kama wakikaa kwa njia hiyo aitawaruhusu kuwa makini kwa yule mtowa khutuba).”

12. Usifanye matangazo yoyote ya kupotea kwa kitu msikitini.[3]

عن أبي هريرة رضي الله عنه قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم من سمع رجلا ينشد ضالة في المسجد فليقل لا ردها الله عليك فإن المساجد لم تبن لهذا (صحيح مسلم، الرقم: 568)

 Sayyidina Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu)  ameripoti kuwa Sayyidina Rasulullah sallallahu alaihi wasallam anasema, ” atakae sikia mtu anatangaza kitu kilichopotea katika msikiti, inabidi amuambie huyo mtu, Allah Ta’ala asirudishe kitu chako kwako.’ Kwa hakika misikiti haijajengwa kwa ajili ya hii kazi.”


[1] ينبغي للجالس في المسجد لانتظار صلاة أو اشتغال بعلم أو لشغل آخر أو لغير ذلك من طاعة ومباح أن ينوي الاعتكاف فإنه يصح عندنا وإن قل زمانه (المجموع شرح المهذب 2/143)

[2] قال المصنف رحمه الله (ويستحب لمن دخل المسجد أن يصلي ركعتين تحية المسجد) … أما حكم المسألة فأجمع العلماء على استحباب تحية المسجد ويكره أن يجلس من غير تحية بلا عذر (المجموع شرح المهذب 3/375)

[3] تكره الخصومة في المسجد ورفع الصوت فيه ونشد الضالة وكذا البيع والشراء والاجارة ونحوها من العقود هذا هو الصحيح المشهور (المجموع شرح المهذب 2/141)

[4] قال أبو عيسى: حديث عبد الله بن عمرو بن العاص حديث حسن

About admin

Check Also

Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu …