Salaam Kwa Nabii ﷺ

Kutokomeza Kwa Umasikini

Sayyidina Samurah Suwaai (radhiallahu anhu), baba wa Sayyidina Jaabir (radhiallahu anhu), ameripoti kwamba: tuliwahi kuwa na Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam) pindi mtu mmoja alikuja kwa Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam) na akauliza, " ewe Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam) !ni tendo gani linalomrizisha Allah subhaana wata'alah zaidi?" Nabii wa Allah-(sallallahu alaihi wasallam) akajibu, "maneno ya ukweli na kutimiza uwaminifu." Nikasema, "ewe Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam)! Nakuomba utuzidishie nasaha (kuhusu matendo yanayo mrizisha Allah subhaana wata'alah)!" Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam) akasema, " swali wakati wa usiku na funga wakati wa jua kali." Kisha nikasema, ewe Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam)! Nakuomba utuzidishie nasaha!" Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam) akasema, " jishughulishe na zikr kwa wingi na nitumie salaam inaondowa umasikini," nikauliza tena, ewe Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam) nakuomba utuzidishie nasaha! Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam) akasema, yule atakae  swalisha  watu basi  afupishe swala,kwa sababu kwenye jamaa  kuna wazee, kuna wagonjwa, vijana na watu kuna ambao wana dharura."

Soma Zaidi »

Kukubalika Kwa Dua

Imepokelewa kutoka kwa Umar (radhiallahu anhu) dua zinabaki zimesimamishwa kati ya mbigu na ardhi. Hazitafika mbinguni Kama salaam haijatumwa kwa Nabii (sallallahu alaihi wasallam) (yaani hakuna uwakika wa kukubalika)."

Soma Zaidi »

Ongezeko la rizki

Sahl bin Sa'd (radhiyallahu ‘anhu) ameripoti kwamba kuna wakati mmoja, sahaba mmoja alimfata Nabii wa allah (sallallahu alaihi wasallam) Na akalalamika juu ya umasikini na ugumu wa kupata rizki. Nabi wa Allah (sallallahu alaihi wasallam) akamuambia huyu sahaba, "pindi unapo ingia nyumbani kwako, kuwepo watu ndani au hata kama hamna watu ndani basi toa salaam. Baada ya hapo nitumie mimi salaam na soma Qul-Huwallah (surah ikhlaas) mara moja". Sahaba akafanya jinsi alivyo amrishwa na Nabii wa allah (sallallahu alaihi wasallam), na Allah subhaana wata'alah akambariki kwa utajiri mwingi na akaanza kutumia kwa majirani na ndugu zake.

Soma Zaidi »

Kupokea Cheti cha Uhuru kutokana na Unafiki na moto wa Jahannam

Anas (radhiyallahu anhu) ameripoti kwamba Nabii wa Allah (sallallahu alaih wasallam) amesema, "yoyote atakae nitumia salaam mara moja, kwa kumlipa Allah subhaana wata'alah atamtumia salamu mara kumi (yaani: ataampa zawadi na atamfariji na rehma zake), na yoyote atakae nitumia salaam mara kumi, Allah subhaana wata'alah atamtumia salaam mara mia (yaani: ataampa zawadi na atamfariji na rehma zake), na yoyote atakae nitumia salaam mara mia, Allah subhaana wata'alah Atamwandikia (cheti) uhuru, katikati ya macho yake mawili, kutokana na unafiki, (na cheti ya) uhuru kutokana na moto wa jahannum, na Allah subhaana wata'alah ataampa heshma na faraja ya kuwa na mashahidi siku ya qiyamah."

Soma Zaidi »

Mahitaji yote ya dunia na ya deeni kutimizw

Habbaan Bin Munqiz (radhiyallahu anhu) ameripoti kwamba sahabi moja aliwahi kumuuliza Nabii wa allah (sallallahu alaih wasallam), "Ewe mjumbe wa Allah (sallallahu alaih wasallam) je nijitolee thuluthi moja ya muda  ambao nimezitenga kufanya dua ili nitume salaam kwako? "Nabii wa allah (sallallahu alaih wasallam) Alijibu, "ndio, kama utapenda." Ule sahabah akauliza, "je nijitolee thuluthi mbili ya muda ambao nimezitenga kufanya dua ili nitume salaam kwako? "Nabii wa allah akajibu tena, "ndio, kama utapenda. "ule sahabah akauliza, "je nijitolee muda wote kukutumia salaam? "Nabii wa allah (sallallahu alaih wasallam) akajibu, "kama utafanya hivyo, Allah subhaana wata'alah Atayatimiza mahitaji yako yote ambayo unayo (na amboyo ungeulizia kwenye dua yako), ikiwa niyakuhusu dunia au aakhera."

Soma Zaidi »

Mahitaji mia kuitimizwa

Hadrat Jaabir (radhiyallahu ‘anhu) ameripoti kwamba Nabii wa allah (sallallahu ‘alaihi wasallam) Alisema, "yoyote atakae nitumia salaam mara mia moja kwa kila siku, Allah ta'ala atatimiza mahitaji zake mia, sabini za aakherah na thalathini za duniani."

Soma Zaidi »