Kumswalia Nabii wa Allah (sallallahu ‘alaihi wasallam) wakati wa Kuingia na Kutoka Msikitini

عن عبد الملك بن سعيد بن سويد قال سمعت أبا حميد أو أبا أسيد الأنصارى يقول قال رسول الله صلى الله عليه وسلم إذا دخل أحدكم المسجد فليسلم على النبى صلى الله عليه وسلم ثم ليقل اللهم افتح لى أبواب رحمتك فإذا خرج فليقل اللهم إنى أسألك من فضلك. (أبو داود الرقم: 465)

Abu Humaid au Abu Usaid (radhiyallahu ‘anhuma) anaripoti kwamba Nabii wa Allah (sallallahu ‘alaihi wasallam) amesema: “Kila mtu anapoingia msikitini, kinabidi mtu atume salaam juu ya Nabii wa Allah (sallallahu ‘alaihi wasallam) na kisha asome dua ifuatayo:

اللَّهُمَّ افْتَحْ لَنَا أَبْوَابَ رَحْمَتِك
Ewe Allah, nifungulie milango ya rehema zako.

Na anapotoka msikitini kinabidi atume  salaam Kwa Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) na kisha asome dua ifuatayo:

اللهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ مِنْ فَضْلِكَ

Ewe Allah, nakuomba fadhila Zako.”

Kupata Msamaha kupitia Kuandika salaa na salaam

Ibnu Abi Sulaimaan (rahimahullah) anataja:

Nilimwona baba yangu katika ndoto baada ya kifo chake. Nilimuuliza, “jinsi gani Allah subhaana wata’ala Alikushughulikia?” Akajibu: “Allah subhaana wata’ala amenisamehe.” Nikauliza, “Ni kwa kitendo gani alichokusamehe?” Yeye
akajibu, “Nilikuwa nikiandika salaa na salaam baada ya jina la Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) katika kila hadith.”

About admin

Check Also

Chanzo cha nuru siku ya Qiyaama

عن ابن عمر رضي الله عنهما قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم زينوا …