Namna ya Kutoa Adhaan ya Alfajiri

Ikiwa mtu atatoa Adhaan ya Alfajiri, basi atatoa adhaan kwa namna ile ile iliyoelezwa. Tofauti pekee ni kwamba mtu atasoma maneno yafuatayo mara mbili baada ya kusema حَيَّ عَلٰى الْفَلَاحْ (Hayya ‘alal falaah):[1]

اَلصَّلَاةُ خَيْرٌ مِّنَ النَّوْمْ

Swalaah ni bora kuliko usingizi.

عن محمد بن عبد الملك بن أبي محذورة عن أبيه عن جده رضي الله عنه قال قلت يا رسول الله علمني سنة الأذان … فإن كان صلاة الصبح قلت الصلاة خير من النوم الصلاة خير من النوم (سنن أبي داود، الرقم: 500)[2]

Sayyiduna Abu Mahzoorah (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba wakati mmoja, alisema kwa Sayyiduna Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam), “Ewe Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam), nifundishe njia ya kisunnah ya kutoa adhaan.” … Sayyiduna Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) akasema: “Ikiwa ni adhaan ya Alfajiri, basi ongeza maneno اَلصَّلَاةُ خَيْرٌ مِّنَ النَّوْمْ (assalaatu khairum minam nawm) mara mbili (baada ya حَيَّ عَلٰى الْفَلَاحْ Hayya ‘alal falaah).


[1] (و) يسن (التثويب) ويقال التثوب بالمثلثة فيهما (في) أذان (الصبح) وهو قوله بعد الحيعلتين الصلاة خير من النوم مرتين (مغني المحتاج 1/328)

التثويب أن يقول في أذان الصبح بعد الحيعلتين الصلاة خير من النوم مرتين، وهو سنة على المذهب الذي قطع به الأكثرون (روضة الطالبين 1/310)

[2] سكت عن هذا الحديث أبو داود والمنذري (مختصر سنن أبي داود 1/202)

About admin

Check Also

Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu …