7. Soma tasbeeh ifuatayo mara tatu au idadi yoyote isiyo ya kugawanyika:
سُبْحَانَ رَبِّيَ الْعَظِيْم
Utukufu ni wa Mola wangu Mkubwa.
8. Baada ya kusoma tasbihi, simama kutoka kwenye rukuu huku ukisema tasmee’:
سَمِعَ اللهُ لِمَنْ حَمِدَهْ
Allah Ta’ala Humsikia mwenye kumsifu.
9. Inua mikono (kama ilivyoelezwa katika takbeeratul ihraam) na iweke pembeni.
10. Soma Tahmid:
رَبَّنَا لَكَ الْحَمْد
Ewe Mola wetu, hakika kwako wewe pekee ndiyo sifa njema.
11. Simama wima kwa tumaaninah (mwili upate utulivu kabisa) kabla ya kuingia kwenye sajdah.