Rukuu na I’tidaal

1. Ukimaliza kusoma Surah Faatihah na Qiraah (Surah nyingine), tulia kwa muda na baada ya hapo inua mikono (kama ilivyoelezwa katika takbeeratul ihraam) huku ukisema takbira na endelea kwa kwenda kwenye rukuu.

Kumbuka: Takbira ya intiqaaliyyah (takbira inayosomwa wakati wa kuhama kutoka kwenye mkao mmoja hadi mwingine) inapaswa kuanza mara tu mtu anapoanza kuhamia mkao unaofuata na ikamilike pale tu anapofikia mkao mpia.

2. Pinda mgongo kidogo tu kwa kiasi ambacho vidole vinaweza kugusa magoti.

3. Weka vidole pamoja.

Kumbuka: Mtu hatoshikilia magoti kikamilifu wala kusambaza vidole mbali mbali. Vile vile, kichwa na mgongo hazitowekwa sawa sawa kwenye mstari (kama inavyofanywa na wanaume wakati wa kufanya rukuu).

4. Weka mikono karibu na upande wa mwili.

5. Vifundo vya miguu vyote miwili viwe pamoja. Ikiwa hii ni vigumu, basi wanapaswa kuwekwa karibu iwezekanavyo.

6. Macho yanapaswa ya angalie kwenye sehemu ya sajda pindi upo kwenye rukuu.

About admin

Check Also

Qa’dah Na Salaam

7. Ikiwa ni qa’dah ya mwisho, basi soma tashahhud, Swalawaat Ebrahimiyyah na baada ya hapo …