Sunna Za Msikiti

4. Nenda msikitini kwa utulivu na kwa njia ya heshima. Usije mbio msikitini na kukimbia.[1]

عن أبي هريرة رضي الله عنه قال سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول إذا أقيمت الصلاة فلا تأتوها تسعون وأتوها تمشون عليكم السكينة فما أدركتم فصلوا وما فاتكم فأتموا (صحيح البخاري، الرقم: 908)

Sayyidina Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) alisema, “Nilimsikia Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) Akiseme, ‘Inapotolewa Iqaamah ya Swalaah, basi usiende kwenye Swalah hali wewe uko Mbio badala yake, nenda ukitembea kwa utulivu. Idaadi yoyote ya Swalah utakayoipata na Imaam, basi swali; na idaadi yenye ulilolikosa, basi itimize (baada ya Imaam kumaliza Swalaah).’”

5. Ingia msikitini katika hali ya udhu. Ni makrooh kuingia msikitini bila udhu.[2]

عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال لا يزال العبد في صلاة ما كان في مصلاه ينتظر الصلاة وتقول الملائكة اللهم اغفر له اللهم ارحمه حتى ينصرف أو يحدث قلت ما يحدث قال يفسو أو يضرط (صحيح مسلم، الرقم: 649)

Sayyidina Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba Sayyidina Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) kasema: “kwa muda wote mtu anakaa kwenye Musalla wake akingoja swala, anapata ujira wa yule aliyekuwa katika Swalaah. Malaika wanaendelea kumuombea dua wakisema, ‘Ewe Allah subhaana wata’ala, msamehe! Ewe Allah ta’ala mrehemu!’ Yeye anaendelea kupokea ujira mpaka atoke msikitini au hadathi Kutokea akiwa ndani ya msikiti.” Sahabi mmoja akauliza, “Vipi hadathi inatokea?” Sayyidina Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) akajibu, “Kupitia kwa upepo (kuvunja udhu).”


[1] قال المصنف رحمه الله (ويستحب لمن قصد الجماعة أن يمشي إليها وعليه السكينة والوقار) … قد ذكرنا أن مذهبنا أن السنة لقاصد الجماعة أن يمشي بسكينة سواء خاف فوت تكبيرة الإحرام أم لا (المجموع شرح المهذب 4/73)

ولو خاف فوت التكبيرة لو لم يسرع لم يسن له الإسراع بل يمشي بسكينة كما لو أمن فوتها لخبر إذا أقيمت الصلاة فلا تأتوها تسعون وأتوها تمشون وعليكم السكينة والوقار فما أدركتم فصلوا وما فاتكم فأتموا (نهاية المحتاج 2/144-145)

[2] ويكره كما في الإحياء دخول المسجد من غير وضوء (نهاية المحتاج 2/120)

ويكره أن يدخل المسجد بغير وضوء (مغني المحتاج 1/510)

About admin

Check Also

Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu …