Sahaabah

Ndoto Ya Sa’d (radhiyallahu ‘anhu) Kabla ya Kusilimu

Sa’d (radhiya allaahu ‘anhu) anasimulia kwamba: Kabla ya kusilimu, niliota ndoto ambayo niliona niko gizani kabisa na kutokuona chochote. Ghafla, mwezi ukatokea ambalo ulianza kumulika usiku. Kisha nikaufuata huo mwanga hadi nikaufikia mwezi. Katika ndoto, niliona watu fulani ambao walikuwa wamenitangulia kuufikia mwezi. Nilimuona Zaid bin Haarithah, ‘Ali bin Abi …

Soma Zaidi »

Ali (Radhiya Allaahu ‘anhu) Akitumwa Na Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) Kusawazisha Makaburi, Kuvunja Masanamu na Kufuta Picha

Ali (radhiya allaahu ‘anhu) anaripoti kwamba katika tukio moja, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alihudhuria janaazah la Sahaabi fulani. Baada ya hapo akawahutubia maswahaabah (radhiya allaahu ‘anhum) waliokuwepo na akasema: “Ni nani miongoni mwenu atakayerejea Madinah Munawwarah, na popote atakapoona sanamu yoyote atalivunja, na popote atakapoliona kaburi lililoinuliwa (juu ya ardhi, …

Soma Zaidi »

Uadilifu Wa Ali (radhiya allaahu ‘anhu)

Ali bin Rabi’ah anasimulia kwamba wakati mmoja, Ja’dah bin Hubairah (radhiya allaahu ‘anhu) alikuja kwa Ali (radhiya allaahu ‘anhu) na akasema, “Ewe Ameer-ul-Mu’mineen! Tunakuta watu wawili wanakujia (na ugomvi wao). Moja kati ya hao wawili wewe ni kipenzi zaidi kwake kuliko hata familia yake na mali yake, alafu yule mwingine …

Soma Zaidi »

Mapenzi Ya Dhati Ya Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) Kwa Ali (radhiya allaahu ‘anhu)

Ali (radhiya allaahu ‘anhu) anaripoti: Kuna wakati moja, nilikuwa mgonjwa. Nikiwa mgonjwa, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alikuja kunitembelea. Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alipoingia nyumbani kwangu, nilikuwa nimejilaza. Aliponiona niko katika hali hio, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alinikaribia na kuvua kitamba aliyokuwa ameivaa kisha akanifunika nacho. Baada ya hapo, alipoona udhaifu …

Soma Zaidi »

Ushujaa Wa Ali (radhiyallahu ‘anhu) Katika Vita Vya Khaibar

Katika tukio la Khaibar, baada ya Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) kukabidhi bendera ya Uislamu kwa Ali (radhiya allaahu anhu), Ali (radhiyallahu anhu) aliliongoza jeshi la Maswahaabah (radhiyallahu anhu) hadi kwenye ngome ya Qamoos. Walipokaribia ngome, shujaa mmoja wa kiyahudi, jina lake Marhab, alitoka ili kuwapinga (waislamu). Marhab alikuwa shujaa maarufu …

Soma Zaidi »

Hofu Ya Ali (radhiya allaahu ‘anhu) Na Akhera

Kumail ibn Ziyad (rahimahullah) anaripoti yafuatayo: Wakati mmoja, nilifuatana na Ali (radhiya allaahu ‘anhu) alipokuwa akitoka katika mji wa Kufah na kuelekea Jabbaan (kijiji nje ya Kufah). Alipofika Jabbaan, Ali (radhiya allaahu ‘anhu) aligeuka kuelekea makaburini na akaita, “Enyi wakazi wa makaburini! Enyi watu ambao miili yenu imeoza! Enyi watu …

Soma Zaidi »

Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) Amemchagua Ali (radhiya allaahu ‘anhu) Kuisimamia Madinah Munawwarah

Katika tukio la Vita vya Tabook, wakati Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) alipokuwa anaondoka kutoka Madinah Munawwarah, alimchagua Ali (radhiya allaahu ‘anhu) kusimamia mambo ya Madinah Munawwarah akiwa hayupo. Kwa hiyo, kwa maelekezo ya Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam), Ali (radhiya allaahu ‘anhu) hakutoka na jeshi, bali alibakia Madinah Munawwarah. Baada ya …

Soma Zaidi »

Ushujaa wa Ali (radhiya allaahu ‘anhu)

Wakati wa Vita vya Uhud, Ali (radhiyallahu ‘anhu) alionyesha ujasiri na ushujaa wa hali ya juu katika kupigana na maadui. Hivyo, yeye binafsi alihusika kuwaua viongozi wanne wa Maquraishi, miongoni mwao akiwa ni Talhah bin Abi Talhah. Baada ya vita, alimkabidhi upanga wake kwa mke wake mheshimiwa, Faatimah (radhiya allaahu …

Soma Zaidi »

Mapenzi ya Ali (radhiya allaahu ‘anhu) kwa Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam)

Wakati mmoja, Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) alikuwa hana chakula na kuhisi njaa. Wakati Ali (radhiya allaahu ‘anhu) alipopata habari kwamba Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) alikuwa akipatwa na njaa, mara moja moyo wake ulijaa na wasiwasi. Hayo yalikuwa mapenzi yake kwa Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) kiasi kwamba hakuweza kupumzika huku akijua …

Soma Zaidi »