Unyenyekevu Wa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu)
Wakati watu walikuwa wakija kwa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) na kumsifu kwa fadhila na baraka kubwa ambazo Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) kamjalia, alikuwa akiwajibu kwa unyenyekevu akisema:
“Mimi ni mtu wa Habsha tu ambaye alikuwa mtumwa jana.” (Tabaqaat ibn sa’d 3/180)