Kuitikia Iqaamah

Itikia iqaamah kama vile unavyo itikiaa adhaan. Kwa hiyo, wakati wa kuitikia  قَدْ قَامَتِ الصَّلاَهْ (qad qaamatiss alaah) basi sema:[1]

أَقَامَهَا اللهُ وَأَدَامَهَا وَجَعَلَنِيْ مِنْ صَالِحِيْ أَهْلِهَا

Allah subhaana  wata’ala aiweke (Swalaah) na aihifadhi na anijaalie niwe miongoni mwa waja wema wanao simamisha swalaah.

عن أبي أمامة أو بعض أصحاب رسول الله صلى الله عليه وسلم أن بلالا أخذ في الإقامة فلما أن قال قد قامت الصلاة قال رسول الله صلى الله عليه وسلم أقامها الله وأدامها (سنن أبي داود، الرقم: 528)[2]

Sayyiduna Abu Umaamah (radhiyallahu ‘anhu) au Sahaabi mwingine anaripoti kwamba kuna wakati mmoja, Sayyiduna Bilaal (radhiyallahu ‘anhu) alikuwa akitoa iqaamah. Alipofikia maneno قَدْ قَامَتِ الصَّلاَهْ  (qad qaamatis swalaah), Sayyiduna Rasulullah (sallallahu  alaihi  wasallam)  akajibu kwa kusema (aqaamahallaahu wa adaamahaa).


[1] وأن يجيب كل من سمع الأذان وإن كان جنبا أو حائضا فيقول مثل قول المؤذن في جميع الأذان والإقامة … وإلا في كلمتي الإقامة فيقول أقامها الله وأدامها وجعلني من صالحي أهلها (روضة الطالبين 1/313)

[2] قال المنذري: في إسناده رجل مجهول وشهر بن حوشب تكلم فيه غير واحد ووثقه الإمام أحمد ويحيى بن معين (مختصر سنن أبي داود 1/210)

About admin

Check Also

Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu …