Matamshi Sahihi ya Maneno ya Adhaan

Wakati wa kutoa adhaan, mtu ajitahidi kutamka maneno kwa usahihi. Katika suala hili, baadhi ya nukta muhimu kuzikumbuka ni:

1. Wakati wa kusema اَللهُ أَكْبَرَ اللهُ أَكْبَرْ ,herufu ر (Raa) katika أَكْبَرْ (Akbar) ya kwanza itasemwa na fat-hah (ــَـ) (kwa kuiunganisha na neno اللهُ (Allahu).

2. Pindi unapo sema أَشْهَدُ أَلَّا إِلٰهَ إِلَّا اللهْ, Neno أَلَّا (Al-laa) inabidi isomwe na mdomo wazi. Vile vile tashdeed (ــّـ) yenyewe ipo juu ya ل (Laam) inabidi isemwe Kwa msisitizo Kwa kukaza sauti ya ل (Laam).

Sukoon (ــْـ) au sakna juu ya ش (Sheen) isomwe vizuri na kuonganishwa na هـ (Haa). Sakna kwenye ش (Sheen) na herufu هـ (Haa) isiachane Kwa kuunganisha herufu هـ (Haa) kwenye ش (Sheen) na kusema “ashadu” bila kutaamka herufu هـ (Haa) kabisa. Kwa hiyo njia sahihi kutamka ni “ash – ha – du”.

3. Pindi unapo sema أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا رَّسُوْلُ اللهْ , Neno أَنَّ (Anna) haitakiwi kuvuta sana tashdeed kwenye ن (Noon) zaidi ya muda wa kusoma ghunnah. Vile vile tashdeed (ــّـ) Kwenye herufu م (Meem) na ر (Raa) haitakiwi pia kuvutwa sana.

4. Pindi unaposema حَيَّ عَلٰى الصَّلَاةْ, Tashdeed (ــّـ) Kwenye herufu ي (Yaa) kwenye neno حَيَّ (Hayya) inatakiwa kusomwa kwa ukamilifu. Ile ي (Yaa) haitakiwi kusomwa bila tashdeed (ــّـ) Kwa kusema “haya” badala ya “hayya”. Vili vile herufu ع (‘ain) kwenye neno على (‘ala) inabidi isemwe vizuri.

Pindi unapoishia mwisho wa neno الصَّلَاةْ (Swalaah), ile ة (Taa) itasemwa na sakna (ــْـ) Na kuwa na sauti ya هـ ( Haa). Haitakiwi mtu kusoma ile ة (Taa) Kwa kusema “hayya ‘alas swalaaht.

Vile vile inabidi kuakikisha Kwamba sauti ya ة (Taa) isifanane na sauti ya herufu ح (Haa).

5. Pindi unaposema حَيَّ عَلٰى الْفَلَاحْ , Wakati unapoishia kwenye neno الْفَلَاحْ (Falaah), hakikisha herufu ح (Haa) inasomwa Kwa usahihi Kwa kuisoma Kama ح (Haa) na sio هـ.

About admin

Check Also

Maneno ya Iqaamah na Njia ya Sunnah ya kutoa Iqaamah

1. Maneno ya iqaamah ni sawa sawa na maneno ya adhaan. Kwa hivyo, wakati wa …