Njia ya Sunna ya kuita adhana.

15. Ikiwa uko mahali nje ya mji ambapo hakuna mtu wakuswali pamoja naye, basi hata kama utaswali peke yako, bado unapaswa kutoa adhaan na iqaamah. Ukitoa adhaan na iqaamah na baada ya hapo ukaswali basi Malaika wataswali pamoja na wewe.[1]

عن عقبة بن عامر رضي الله عنه قال سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول يعجب ربك من راعي غنم في رأس شظية الجبل يؤذن بالصلاة ويصلي فيقول الله عز وجل انظروا إلى عبدي هذا يؤذن ويقيم الصلاة يخاف مني قد غفرت لعبدي وأدخلته الجنة (سنن النسائي، الرقم: 666)[2]

Sayyiduna Uqbah bin Aamir (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti, “Nilimsikia Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) akisema, ‘Allah subhaana wata’ala anafurahi pindi mchungaji wa mbuzi na kondoo ambaye yuko (peke yake) juu ya kilele cha mlima anatoa adhaan kisha anaswali. Kwa hivyo, Allah subhaana wata’ala anasema, Tazama mja wangu huyu! Anatoa adhaan na kusimamisha Swalaah huku akiniogopa! Hakika Nimemsamehe mja wangu na mimi (nimeamuru kwamba) nitamuingiza peponi!’

عن سلمان الفارسي رضي الله عنه قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم إذا كان الرجل بأرض قي فحانت الصلاة فليتوضأ فإن لم يجد ماء فليتيمم فإن أقام صلى معه ملكاه وإن أذن وأقام صلى خلفه من جنود الله ما لا يرى طرفاه (الترغيب والترهيب، الرقم: 387)[3]

Sayyiduna Salmaan Al-Faarsi (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba Sayyiduna Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) amesema: “Mtu anapokuwa (peke yake) katika jangwa na wakati wa Swalaah unaingia, basi anatakiwa kutawadha. Ikiwa hawezi kupata maji basi afanye tayammam. Ikiwa yeye Anatoa iqaamah (kabla ya kuswali), Malaika wake wawili wataswali naye, na ikiwa atatoa adhaan na iqaamah (kabla ya kuswali), majeshi makubwa kama haya ya Allah subhaana wata’ala (Malaika) wataswali nyuma ambao mwisho wa majeshi haya hayawezi kuonekana.”

16. Kama Swalaah nyingi za qadhaa zinaswaliwa kwa pamoja basi adhaan moja itatolewa tu kwa ajili ya Swalaah ya kwanza iliyokoswa. Lakini iqaamah tofauti itolewe kwa kila Swalaah.[4]

عن أبي عبيدة بن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه قال قال عبد الله إن المشركين شغلوا رسول الله صلى الله عليه وسلم عن أربع صلوات يوم الخندق حتى ذهب من الليل ما شاء الله فأمر بلالا فأذن ثم أقام فصلى الظهر ثم أقام فصلى العصر ثم أقام فصلى المغرب ثم أقام فصلى العشاء (سنن الترمذي، الرقم: 179)[5]

Sayyidina Abu Ubaidah (rahimahullah) anaripoti kwamba baba yake, Sayyiduna Abdullah bin Mas’uud (radhiyallahu ‘anhu) ametaja, “Katika tukio la Vita vya Khandaq (Vita vya Handaki), makafiri walimuweka Rasulullah (na Waumini) kushughulika (kupitia kupigana) mpaka zikakosekana Swalaah nne na kipindi cha usiku ulikuwa amepita. Sayyiduna Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) kisha akaamuru Bilaal (radhiyallahu ‘anhu) kutoa adhaan. Baada ya kutoa adhaan Bilaal (radhiyallahu ‘anhu) alitoa iqaamah na wakaswali qadhaa wa Swalaah ya Adhuhuri. Baada ya hapo, Bilaal (radhiyallahu ‘anhu) alitoa iqaamah na wakaswali qadhaa ya Swalaah ya Asr. Baada ya hapo, Bilaal (radhiyallahu ‘anhu) akatoa Iqaamah na wakaswali qadhaa ya Swalaah ya Maghrib. Mwisho Bilaal akatoa Iqaamah na (radhiyallahu ‘anhu) wakaswali Ishaa.”

Kumbuka: Swalaah ya ishaa sio kama haikuswaliwa bali ilitekelezwa baadaye usiko sio muda wa kawaida. Kwa ajili hiyo, Swalaah ya Esha ilijumuishwa pia na Swalaah nyingine zilizokoswa.


[1] المنفرد في صحراء أو بلد يؤذن على المذهب والمنصوص في الجديد والقديم لإطلاق الأحاديث (المجموع شرح المهذب 3/65)

في مذاهب العلماء في الأذان والإقامة مذهبنا المشهور أنهما سنة لكل الصلوات في الحضر والسفر للجماعة والمنفرد (المجموع شرح المهذب 3/63)

[2] عن عقبة بن عامر قال سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول يعجب ربكم من راعي غنم في رأس شظية بجبل يؤذن بالصلاة ويصلي فيقول الله عز وجل انظروا إلى عبدي هذا يؤذن ويقيم الصلاة يخاف مني قد غفرت لعبدي وأدخلته الجنة (سنن أبي داود: الرقم: 1203)

قال المنذري: رجال إسناده ثقات (مختصر سنن أبي داود 1/385)

[3] قال المنذري: رواه عبد الرزاق في كتابه عن ابن التميمي عن أبيه عن أبي عثمان النهدي عنه القي بكسر القاف وتشديد الياء هي الأرض القفر

[4] أما حكم المسألة فإذا أراد قضاء فوائت دفعة واحدة أقام لكل واحدة بلا خلاف ولا خلاف أنه لا يؤذن لغير الأولى منهن وهل يؤذن للأولى فيه الأقوال الثلاثة التي ذكرها المصنف بدلائلها أصحها عند جمهور الأصحاب يؤذن … فهذا هو الصحيح الذي جاءت به الأحاديث الصحيحة ولا يغتر بتصحيح الرافعي وغيره منع الاذان (المجموع شرح المهذب 3/64-65)

[5] قال أبو عيسى: وفي الباب عن أبي سعيد وجابر حديث عبد الله ليس بإسناده بأس إلا أن أبا عبيدة لم يسمع من عبد الله

قال الحافظ في الفتح (2/82): وفي قوله أربع تجوز لأن العشاء لم تكن فاتت

About admin

Check Also

Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu …