Dalili Za Qiyaamah Part 4

Dalili Kumi Kubwa Za Qiyamah

Kama jinsi kuna dalili nyingi ndogo za Qiyaamah zilizorekodiwa katika Ahaadith, hivyo hivyo kuna dalili nyingi kubwa ambazo pia zimetajwa katika Ahaadith. Dalili hizi kubwa ni matukio muhimu ambayo yatatokea ulimwenguni kabla ya Qiyaamah na itatangaza ukaribu wa Qiyaamah. Muhadditheen wame eleza kuja kwa Mahdi (Radhiyallahu ‘Anhu) ni dalili ya kwanza ya Qiyaamah. (Ishaa’ah pg. 191)

Katika dalili hizi kubwa za Qiyamah, kuna dalili kumi ambazo zimeelezwa na Rasulullah (Sallallahu ‘Alaihi Wasallam) katika Hadith ifuatayo. Ikiwa mtu atatafakari juu ya dalili hizi kumi, atatambua kuwa ni ya ukubwa kiasi kwamba athari zake zitaingia ulimwengu wote au sehemu kubwa nyingi ya ulimwengu.

Huzaifah bin Usaid (Radhiyallahu ‘Anhu) anaripoti, “Katika tukio moja, Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam) alitujia sisi maswahaabah (Radhiyallahu ‘Anhum), wakati tukishiriki katika majadiliano. Rasulullah (Sallallahu ‘Alaihi Wasallam) aliuliza kutoka kwetu, “Mnajadili nini?” Tulijibu, “Tunazungumzia kuhusu tukio la Qiyaamah.” Kusikia haya, Rasulullah (Sallallahu ‘Alaihi Wasallam) alisema, “Kwa kweli, Qiyaamah haitatokea kamwe hadi utaona kabla yake dalili kumi kubwa. ”

“Rasulullah (Sallallahu ‘Alaihi Wasallam) kisha akataja dalili hizi kumi kuwa: moshi (hii ni aina ya ukungu au moshi ambao utashuka duniani kutoka angani ambayo Waislamu watapata homa na makafiri watazimia), Dajjaal kutokea, mnyama kutokea, jua kutoka magharibi, Nabi Isa (‘Alaihis Salaam) kushuka, Yajooj na Ma’jooj kutokea, ardhi kuzama mara tatu duniani; Kuzama mashariki, kuzama magharibi na kuzama katika peninsula ya Arabia. Dalili ya mwisho itakuwa moto ambao utatokea Yemen na kuwaongoza watu kuelekea katika uwanja wa kufufuliwa (Syria). ” (Saheeh Muslim #2901)

Katika dalili hizi kumi kubwa zilizotajwa katika Hadith hii, ya kwanza kutokea itakuwa kutokea kwa Dajjaal.

Kutokea Kwa Dajjaal

Imeripotiwa katika Hadith kwamba tangu mwanzo wa wakati hadi kuja kwa Qiyamah, fitnah ya Dajjal itakuwa kati ya majaribio makubwa ambayo ulimwengu utashuhudia. Rasulullah (Sallallahu ‘Alaihi Wasallam) alisema, “Tangu kuumbwa kwa Nabi Aadam (‘ Alaihis salaam) hadi siku ya Qiyaamah, hakuna fitna ambayo itakuwa kubwa kuliko fitna ya Dajjaal.” (Mu’jam Kabeer #451)

Kwa kuwa Dajjaal atatokea katika Ummah huu- Ummah wa Rasulullah (Sallallahu ‘Alaihi Wasallam) – watalazimika kugombana na fitnah hii kubwa. Kiwango cha fitnah ulimwenguni cha Dajjaal kinaweza kujilakana kwa kuwa kila Nabi alimjulisha Ummah wake kuhusu Dajjaal kutokea na madhara makubwa ambayo atasababisha ulimwenguni.

Abdullah bin Umar (Radhiyallahu ‘Anhuma) anaripoti kwamba wakati moja, Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam) alisema, “Kwa kweli ninakuonya juu ya Dajjaal, na hakukuwa Nabi yoyote ambaye hakuwaonya watu wake kuhusu Dajjaal, hadi Nabi Nuh (Alaihis salaam) aliwaonya watu wake kuhusu Dajjaal. Lakini nitakuambia kitu cha ziada kuhusu Dajjaal ambacho hakuna Nabi aliwaambia watu wake – eleweni vizuri kuwa Dajjaal ana kasoro katika jicho moja, na Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’ala) sio mtu ambaye ana kasoro katika jicho moja (i.e. yuko huru kwa kasoro zote). ” (Sunan Tirmizi #2235)

Dajjaal ni nani?

Baadhi ya watu wanamaoni kwamba Dajjaal ni mfumo wa ulimwengu na wengine wanahisi kuwa Dajjaal ni Jini. Bado kuna kundi la tatu ambalo linahisi kuwa Dajjaal ni mchanganyiko wa mwanadamu na Jinn. Lakini, imani ya Ahlus Sunnah Wal Jamaa’ah ni kwamba Dajjaal ni mwanadamu maalum ambaye atatokea kwa wakati maalum ulimwenguni. Imani ya Ahlus Sunnah Wal Jamaa’ah imethibitishwa kutoka Ahaadith nyingi za Rasulullah (Sallallahu ‘Alaihi Wasallam).

Insha Allah, katika sehemu zijazo, tutajadili hizo Ahaadith ambazo zinathibitisha imani ya Ahlus Sunnah Wal Jamaa’ah.

About admin

Check Also

Dalili Za Qiyaamah 1

Ndani ya hadith Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alikuwa ametabiri matukio yatakayotokea kabla ya Qiyaamah. Aliutahadharisha …