Hofo Ya Abdur Rahman bin Auf (Radhiyallahu ‘Anhu) Kutoa Hesabu

Naufal bin Iyaas Al Huzali (Rahimahullah) anasimulia:

‘Tulikuwa tukikaa na Abdur Rahman bin Auf (Radhiyallahu’ Anhu), na alikuwa ni rafiki mzuri sana. Siku moja, alitupeleka nyumbani kwake kula. Wakati tulikaa chini na sahani ya chakula iliyo na nyama na mkate ililetwa mbele yetu, alianza kulia.

Tulimuuliza, “Ni nini kinachokusababisha kulia ehh Abu Muhammad?” Akajibu, “Sababu ya mini kulia ni kwamba Rasulullah (Sallallahu ‘Alaihi Wasallam) aliiacha dunia kwa hali kwamba yeye wala familia yake hawakula mkate hadi kujaza tumbo zao (wakati wa uhai wake). Ninaogopa isiwe kuwa kwamba tunaachwa nyuma (ulimwenguni ili kufurahiya fadhila hizi) na badala ya hili, tutanyimwa fadhila za Akhera.” (Isaabah 4/292)

About admin

Check Also

Tamaa kubwa ya Saeed bin Zaid (Radhiyallahu ‘Anhu) kutoa maisha yake katika njia ya Allah Ta’ala

Wakati mji wa Damascus ulipofikia mikononi mwa Waislamu, Abu Ubaidah (Radhiyallahu ‘Anhu) – Kamanda wa …