Hofu Ya Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mali ya Dunia isimfanye Kuto kumcha Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’alah)

Wakati mmoja, Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu) alipokea dirham laki saba kutoka Hadhramawt. Usiku ule, alipopumzika ili alale, hakutulia, akigeuka huku na huko.

Mke wake kuona wasiwasi wake, aliuliza, “Ni nini kinakusumbua?” Akajibu, “Mtu atawezaje kumfikiria Mola wake wakati ana mali nyingi nyumbani kwake? (yaani nahofia kuwa mali hii itasababisha nighafilike na kumsahahu Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’alah) na kuto kumkumbuka)”

Mke wake mheshimiwa alipendekeza azigawe fedha hizo miongoni mwa Maswahabah (Radhiya Allaahu ‘anhum) wa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam). Kusikia hivyo, Talhah (Radhiyallahu ‘anhu) alifarijika na akasema, “Mwenyezi Mungu akurehemu! Hakika wewe ni mwanamke mwema, mwongofu, na binti wa mtu mwema, mwongofu.” Alikuwa Ummu Kulthum, binti wa Abu Bakr (Radhiyallahu ‘anhu).

Asubuhi iliyofuata, aligawa mali kati ya Maswahabah Muhajirina na Ansar (Radhiyallahu ‘anhum). Miongoni mwa Maswahaba aliowapelekea mali hii ni Ali (Radhiya Allaahu ‘anhu).

Mke wake alipomuona akitumia mali yote kwa maswahaabah (Radhiya Allaahu ‘anhum), alimwambia: “Je kuna mali yoyote iliobaki ya kwetu (ili tutekeleze mahitaji zetu)? Akamwambia mke wake kuhifadhi mali iliyobaki, ambayo ilikuwa takriban dirham elfu moja. (Siyaru A’alamin Nubala 3/24)

About admin

Check Also

Uhuru wa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) na hamu ya Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam) kwa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) kuwa huru

Wakati mmoja, wakati akizungumza kuhusu Bilaal (Radhiyallahu 'Anhu), Sa'eed bin Musayyib (Rahimahullah) alisema:

Tamaa ya kuwa muisilamu ilikuwa kubwa sana moyoni mwa Bilal (Radi Allahu 'Anhu). Alikuwa akiwekwa chini na kuteswa katika mikono ya makafiri. Wakati wowote makafiri wangejaribu kumlazimisha kuachana na Uislamu, angekataa kwa nguvu na kutangaza waziwazi "Allah Allah" (yaani Allah Ta'ala ndiye mungu pekee anayestahili kuabudiwa).

Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) kisha alikutana na Abu Bakr (Radhiyallahu' Anhu) na alionyesha hamu yake akisema, "Ikiwa tu tungekuwa na mali ambayo tunaweza kumnunua Bilaal (na kumwachisha huru)!" Baada ya hapo, Abu Bakr (Radhiyallahu 'Anhu) alimkaribia 'Abbaas (Radhiyallahu' Anhu) akamwambia, "Nenda umnunue Bilaal kwa niaba yangu."