Uaminifu Mkubwa Wa Abu Ubaidah bin Jarrah (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Baada ya kusilimu, watu wa Najraan walikuja kwa Mtume (Sallallahu ‘alaihi wasallam) na wakamwomba awapelekee mtu mwaminifu (anayeweza kuwafundisha Dini).

Mtume (Sallallahu ‘alaihi wasallam) akawaambia:

لأبعثن إليكم رجلا أمينا حق أمين

“Nitawatumia mtu mwaminifu, hakika ni mwaminifu sana.”

Katika hatua hiyo, Maswahaabah (Radhiya Allaahu ‘anhum) waliokuwepo wote walitamani kuwa wapokezi wa bashara hii ya Mtume (Sallallahu ‘alaihi wasallam). Kisha Rasulullah (Sallallahu ‘alaihi wasallam) akamchagua Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwenda kwa watu wa Najraan na kuwafundisha dini.

Aliposimama Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu) na kukaribia kuondoka, Mtume (Sallallahu ‘alaihi wasallam) alisema maneno haya kuhusu yeye, “Mtu huyu ndiye muaminifu (maalum) wa Ummah huu”. (Sahih Bukhaari #3480- 3481)

Maelezo: Sifa ya uaminifu ulikuwa ni alama ya Maswahaba wote. Hata hivyo, kwa sababu ya sifa hii kuwa bora zaidi katika maisha ya Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu), Rasulullah (Sallallahu ‘alaihi wasallam) alimpa cheo hiki maalum.

About admin

Check Also

Uhuru wa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) na hamu ya Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam) kwa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) kuwa huru

Wakati mmoja, wakati akizungumza kuhusu Bilaal (Radhiyallahu 'Anhu), Sa'eed bin Musayyib (Rahimahullah) alisema:

Tamaa ya kuwa muisilamu ilikuwa kubwa sana moyoni mwa Bilal (Radi Allahu 'Anhu). Alikuwa akiwekwa chini na kuteswa katika mikono ya makafiri. Wakati wowote makafiri wangejaribu kumlazimisha kuachana na Uislamu, angekataa kwa nguvu na kutangaza waziwazi "Allah Allah" (yaani Allah Ta'ala ndiye mungu pekee anayestahili kuabudiwa).

Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) kisha alikutana na Abu Bakr (Radhiyallahu' Anhu) na alionyesha hamu yake akisema, "Ikiwa tu tungekuwa na mali ambayo tunaweza kumnunua Bilaal (na kumwachisha huru)!" Baada ya hapo, Abu Bakr (Radhiyallahu 'Anhu) alimkaribia 'Abbaas (Radhiyallahu' Anhu) akamwambia, "Nenda umnunue Bilaal kwa niaba yangu."