Kushiriki katika Vita vya Badr

Ismaa’il bin Abi Khaalid anasimulia kwamba Bahiyy (rahimahullah) alisema: “Wapanda farasi walikuwa wawili tu wakipigana katika Jihaad kwenye tukio la Badr. Mmoja wao alikuwa Zubair (Radhiya Allaahu ‘anhu), ambaye alikuwa akipigana upande wa kulia, na mwingine alikuwa Miqdad bin Aswad (Radhiya Allaahu ‘anhu), ambaye alikuwa akipigana upande wa kushoto.

Hishaam bin ‘Urwah anasimulia kwamba baba yake, ‘Urwah (rahimahullah), alisema, “Zubair (Radhiya Allaahu ‘anhu) alikuwa amevaa kilemba cha njano Siku ya Badr. Jibreel (‘Alayhis Salaam) kisha akashuka akifanana na Zubair (Radhiya Allaahu ‘anhu) yaani Jibreel (alaihis salaam) pia alikuwa amevaa kilemba cha njano.”
(Siyar A’laam min Nubalaa 3/29)

About admin

Check Also

Uaminifu Mkubwa Wa Abu Ubaidah bin Jarrah (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Baada ya kusilimu, watu wa Najraan walikuja kwa Mtume (Sallallahu ‘alaihi wasallam) na wakamwomba awapelekee …