Kuwatembelea Wagonjwa

Dini ya Uislamu inatetea na kuamrisha mtu kutimiza haki anazo daiwa na Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’aala) na haki anazo daiwa na waja wa Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’aala). Kuhusu haki anazodaiwa na waja wa Allah Ta’ala, hizi zinaweza kugawanywa katika aina mbili za haki.

Aina ya kwanza ni zile haki ambazo ni maalum kwa kila mtu k.m. haki ambazo mtu anazo daiwa na wazazi wake, ndugu, majirani, nk.

Aina ya pili ni zile haki zinazowahusu waislamu wote kwa ujumla. Kuhusiana na aina hii, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) ameeleza katika Hadithi kwamba kila Muislamu ana haki sita juu ya muislamu mwenzake. Miongoni mwa haki hizi sita mmoja kati yake ni mtu kumtembelea ndugu yake Mwislamu wakati anaumwa.

Ali (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alisema, “Muislamu ana haki sita juu ya ndugu yake Muislamu. Akikutana naye amsalimie (kwa salaam); akimwalika basi akubali mwaliko wake; anapopiga chafya (na kusema alhamdulillah), ajibu chafya yake kwa kusema ‘Yarhamukallah’; mtu akiumwa basi amtembelee; mtu akifariki basi ahudhurie janaazah yake; na anapaswa kumpendelea ndugu yake kile anachojipendea yeye mwenyewe.”

About admin

Check Also

Dua Baada Ya Kula 1

Dua ya kwanza: Sifa zote ni za Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata'ala) ambaye alitupa chakula na vinywaji na kutufanya Waislamu.

Dua ya pili Sifa zote ni za Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata'ala) ambaye alinipa chakula hiki kula, na alinipa bila juhudi yoyote au jitihada kutoka upande wangu.

Maelezo: Mu'aadh bin Anas (Radhiyallahu anhu) anaripoti kwamba Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alisema, "Yoyote anayekula chakula chochote na baada ya hapo anasoma Dua iliyotajwa hapo juu, dhambi zake zilizopita na za baadaye (ndogo) zitasamehewa. "