Sunna Na Adabuza Za Dua 2

2. Unapoomba dua, inua mikono yako sambamba na kifua chako.

Salmaan Faarsi (radhiyallahu ‘anhu) anasema kwamba Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) alisema, “Hakika Allah Ta’ala ndiye mtukufu zaidi na mkarimu zaidi. Heshima yake ni kiasi kwamba anajisikia ni kinyume na ukubwa na rehma yake kumwachia yule anayeinua mikono yake kwa ajili ya kumuomba aende mikono mitupu.”

3. Unapoinua mikono yako katika dua, viganja vyako vielekee juu, kuelekea mbinguni.

Maalik bin Yasaar (radhiyallahu ‘anhu) anasema kwamba Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) alisema, “Wakati wa kumuomba Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’aala), basi muombeni kwa kutumia viganja vyenu vikitazama juu (yaani kuelekea mbinguni). Msielekeze viganja vyenu chini (yaani ardhini).

4. Acha nafasi kidogo kati ya mikono yako miwili.

5. Wakati wa kuomba dua, onyesha kutoweza kwako mwenyewe na udhaifu wako, na umuombe Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’aala) kwa sauti ya upole na unyenyekevu kamili.

وَاذۡکُرۡ رَّبَّکَ فِیۡ نَفۡسِکَ تَضَرُّعًا وَّخِیۡفَة وَّدُوۡنَ الۡجَهرِ مِنَ الۡقَوۡلِ بِالۡغُدُوِّ وَالۡاٰصَالِ وَلَا تَکُنۡ مِّنَ الۡغٰفِلِیۡنَ ﴿۲۰۵﴾

Na muombe Mola wako ndani yako kwa unyenyekevu na kwa khofu bila kupaza sauti asubuhi na jioni. Na usiwe miongoni mwa walioghafilika.

About admin

Check Also

Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu …