Ali (Radhiya Allaahu ‘anhu) Akitumwa Na Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) Kusawazisha Makaburi, Kuvunja Masanamu na Kufuta Picha

Ali (radhiya allaahu ‘anhu) anaripoti kwamba katika tukio moja, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alihudhuria janaazah la Sahaabi fulani. Baada ya hapo akawahutubia maswahaabah (radhiya allaahu ‘anhum) waliokuwepo na akasema: “Ni nani miongoni mwenu atakayerejea Madinah Munawwarah, na popote atakapoona sanamu yoyote atalivunja, na popote atakapoliona kaburi lililoinuliwa (juu ya ardhi, au lina muundo uliojengwa juu yake basi ataliweka sawa (kwa urefu sahihi), na popote atakapoona picha yoyote (ya vitu vilivyo hai), basi ataiharibu mara moja?”

Kusikia hivyo, Sahaabi mmoja alijitolea akisema, “Nitafanya hivyo, ewe Mtume wa Allah (sallallahu ‘alaihi wasallam)!” Hata hivyo, kabla ya kuingia mjini, aliingiwa na khofu ya watu wake, na hivyo akarudi kwa Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) na akaeleza kutoweza kwake kutimiza kazi hiyo. Ali (radhiya allaahu ‘anhu) alikuwepo, na akamwambia Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam), “Nitakwenda, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (sallallahu ‘alaihi wasallam)!”

Ali (radhiya allaahu ‘anhu) kisha akaenda Madinah Munawwarah na kukamilisha kazi aliyokabidhiwa. Aliporudi, alimwambia Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam), “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu (sallallahu ‘alaihi wasallam)! Sikuacha mjini sanamu yoyote, isipokuwa nililivunja, wala kaburi (lililoinuliwa juu ya urefu sahihi), isipokuwa nililisawazisha (kwa urefu sahihi), wala picha yoyote (ya vitu venye uhai), isipokuwa niliviharibu vyote.”

Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) akasema: “Mwenye kurudi kufanya jambo lolote katika mambo haya (yaani. kuyainua makaburi juu ya urefu sahihi au kujenga juu yake, au kutengeneza picha za vitu vilivyo hai), basi ameonyesha kutokujali kabisa na kutokushukuru kwa yale yaliyoteremshwa kwa Muhammad (sallallahu ‘alaihi wasallam) (yaani ameonyesha kutozishukuru sheria za Dini ambazo ziliteremshwa kwa Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam)).”

Kutokana na tukio hili, tunaona ushujaa wa hali ya juu na ujasiri wa kipekee wa Ali (radhiya allaahu ‘anhu), pamoja na shauku yake ya kutimiza daima amri iliyobarikiwa ya Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam). (Musnad Ahmed #657)

About admin

Check Also

Mshale Wa Kwanza Kurushwa kwa Ajili Ya Uislamu

Sa’d (radhiya allaahu ‘anhu) alikuwa miongoni la kundi la Maswahabah ambao Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) …