Uadilifu Wa Ali (radhiya allaahu ‘anhu)

Ali bin Rabi’ah anasimulia kwamba wakati mmoja, Ja’dah bin Hubairah (radhiya allaahu ‘anhu) alikuja kwa Ali (radhiya allaahu ‘anhu) na akasema, “Ewe Ameer-ul-Mu’mineen! Tunakuta watu wawili wanakujia (na ugomvi wao). Moja kati ya hao wawili wewe ni kipenzi zaidi kwake kuliko hata familia yake na mali yake, alafu yule mwingine kama angeweza kukuchinja basi angefanya hivyo (kwa uadui wake kwako). Lakini, licha ya hayo, unatoa hukumu kumpendelea yule anayekuchukia na sio yule anayekupenda!”

Aliposikia hivyo, Ali (radhiya allaahu ‘anhu) alipiga kidogo kifua cha Ja’dah (radhiya allaahu ‘anhu) na mkono wake (kutokana na mapenzi na ili kuvuta mazingatio yake kwa yale aliyokuwa akitaka kumwambia) kisha akasema, “Lau hukumu ingekuwa kupitia uhusiano nilionao na watu, basi mimi ningeweza kuamua kwa niaba ya yule ninayemtaka. Lakini, hukumu inatokana na amri ya Allah Ta‘ala (na katika kumpendelea yule aliye juu ya haq. Kwa kuwa mtu anayenichukia yupo kwenye haq, itabidi nitoe hukumu upande wake).” (Al-Bidaayah Wan-Nihaayah 11/108)

About admin

Check Also

Uhuru wa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) na hamu ya Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam) kwa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) kuwa huru

Wakati mmoja, wakati akizungumza kuhusu Bilaal (Radhiyallahu 'Anhu), Sa'eed bin Musayyib (Rahimahullah) alisema:

Tamaa ya kuwa muisilamu ilikuwa kubwa sana moyoni mwa Bilal (Radi Allahu 'Anhu). Alikuwa akiwekwa chini na kuteswa katika mikono ya makafiri. Wakati wowote makafiri wangejaribu kumlazimisha kuachana na Uislamu, angekataa kwa nguvu na kutangaza waziwazi "Allah Allah" (yaani Allah Ta'ala ndiye mungu pekee anayestahili kuabudiwa).

Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) kisha alikutana na Abu Bakr (Radhiyallahu' Anhu) na alionyesha hamu yake akisema, "Ikiwa tu tungekuwa na mali ambayo tunaweza kumnunua Bilaal (na kumwachisha huru)!" Baada ya hapo, Abu Bakr (Radhiyallahu 'Anhu) alimkaribia 'Abbaas (Radhiyallahu' Anhu) akamwambia, "Nenda umnunue Bilaal kwa niaba yangu."