Mapenzi Ya Dhati Ya Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) Kwa Ali (radhiya allaahu ‘anhu)

Ali (radhiya allaahu ‘anhu) anaripoti:

Kuna wakati moja, nilikuwa mgonjwa. Nikiwa mgonjwa, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alikuja kunitembelea. Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alipoingia nyumbani kwangu, nilikuwa nimejilaza. Aliponiona niko katika hali hio, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alinikaribia na kuvua kitamba aliyokuwa ameivaa kisha akanifunika nacho. Baada ya hapo, alipoona udhaifu wangu, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alisimama na akaenda msikitini kuswali nafl. Baada ya kuswali, alimuomba Allah Ta’ala anibariki na shifaa.

Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) akanijia na kuchukuwa kitamba chake na akaniambia: “Simama ewe mtoto wa Abu Taalib, kwa sababu umeponywa!” Nilisimama na kujikuta nimepona kabisa. Nilijikuta katika hali ambayo hakuna dalili ya ugonjwa au udhaifu uliobaki katika mwili wangu.

Kisha Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) akasema: “Kila nilipomuomba Allah Ta’ala, alikubali dua yangu na akanipa nilichokuwa nimekiomba. (Katika kipindi hiki) chochote nilichojiulizia mwenyewe, pia nilikuombea wewe, (pamoja na shifaa yako).” (Fadhaa’il-ul-Khulafaa li-Abi Nu’aim #78)

Kutokana na tukio hili, tunaona mapenzi makubwa aliyokuwa nayo Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) kwa Ali (radhiya allaahu ‘anhu). Vile vile tunafahamu kuwa Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) ametufundisha kupitia kitendo chake cha baraka kwamba tunapoumwa basi tumuelekee Allah Ta’ala kwenye dua tukimuomba shifaa kwa sababu kila kitu kimo ndani ya uwezo wa Allah Ta’ala.

About admin

Check Also

Uhuru wa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) na hamu ya Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam) kwa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) kuwa huru

Wakati mmoja, wakati akizungumza kuhusu Bilaal (Radhiyallahu 'Anhu), Sa'eed bin Musayyib (Rahimahullah) alisema:

Tamaa ya kuwa muisilamu ilikuwa kubwa sana moyoni mwa Bilal (Radi Allahu 'Anhu). Alikuwa akiwekwa chini na kuteswa katika mikono ya makafiri. Wakati wowote makafiri wangejaribu kumlazimisha kuachana na Uislamu, angekataa kwa nguvu na kutangaza waziwazi "Allah Allah" (yaani Allah Ta'ala ndiye mungu pekee anayestahili kuabudiwa).

Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) kisha alikutana na Abu Bakr (Radhiyallahu' Anhu) na alionyesha hamu yake akisema, "Ikiwa tu tungekuwa na mali ambayo tunaweza kumnunua Bilaal (na kumwachisha huru)!" Baada ya hapo, Abu Bakr (Radhiyallahu 'Anhu) alimkaribia 'Abbaas (Radhiyallahu' Anhu) akamwambia, "Nenda umnunue Bilaal kwa niaba yangu."