Sunnah na Adabu Za Kusoma Qur’an Takatifu 2

6. Inajuzu kusoma Quran Takatifu kwenye simu bila wudhu. Lakini, mtu apaswi kuweka mkono wake au kidole chake kwenye sehemu hiyo ya skrini ambapo aya za Qur’an zinaonekana.[1]

Maelezo: Ikumbukwe kwamba ingawa kusoma Qur’an kutumia simu inaruhusiwa, kusoma Qur’an kwa njia ya asili ni bora zaidi kwa sababu ndio njia asilia Qur’an Takatifu ilivyokuwa inasomwa, na kuna heshima zaidi katika kusoma Quran kwa namna hii.

Kinyume chake, kusoma Qur’an kutumia simu aijahimizwa kwa sababu simu, mara nyingi, ina picha za vitu vilivyo hai na madhambi mengi yanafanywa kupitia simu. Kwa hivyo, hii inasababisha heshima ya Qur’an Takatifu kuathiriwa. Kwa hivyo, ili kusimamisha haki za Qur’an Takatifu na kuionyesha heshima ya hali ya juu inayostahiki, inahimizwa sana kwamba Qur’an Takatifu isomwe kwa njia ya asili kwa kuangalia ndani ya Qur’an Takatifu na kuisoma katika hali ukiwa na wudhu.[2]

7. Tenga muda fulani kila siku kwa ajili ya tilawat (kisomo) cha Quran Takatifu.[3]

Ibnu Umar (radhiyallahu ‘anhuma) anaripoti kwamba Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alisema: “Hakika nyoyo hizi zina kutu kama vile chuma unapata kutu wakati maji yanapoigusa.” Maswahabah (radhiyallahu ‘anhum) wakauliza, “ewe Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam), ni ipi njia ya kuitakasa?” Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) akajibu: “Kukumbuka kifo mara kwa mara na kusoma Qur’an Takatifu.[4]

8. Moja ya haki za Qur’an Takatifu ni kutafakari juu ya maudhui na maana yake ili kutekeleza maamrisho ya Qur’an Takatifu kwa usahihi. Kwa hivyo, pamoja na kusoma Qur’an Takatifu, mtu anapaswa pia kujitahidi kujifunza maana ya surah mbalimbali za Quraan Takatifu. Hili linapaswa kufanywa chini ya ‘Aalim au Sheikhe kamili. Mtu hatakiwi kujisomea na kujifunza mwenyewe.[5]

 أَفَلَا يَتَدَبَّرُونَ الْقُرْآنَ أَمْ عَلَىٰ قُلُوبٍ أَقْفَالُهَا ‎﴿٢٤﴾‏

Kisha Je hawaitafakari Qur’an, au wamewekwa kufuli juu ya nyoyo (zao)? [6] 


[1] المحدث لا يمس المصحف ولا الدرهم الذي كتب عليه القرآن لقوله تعالى: لا يمسه إلا المطهرون (المحيط البرهاني 1/77)

[2] تعظيم القرآن والفقه واجب (فتاوى قاضيخان 3/261)

وأطال الإمام الكلام في هذا المقام بما لا يخفى حاله على من راجعه نعم لا شك في دلالة الآية على عظم شأن القرآن ومقتضى ذلك الاعتناء بشأنه ولا ينحصر الاعتناء بمنع غير الطاهر عن مسه بل يكون بأشياء كثيرة كالإكثار من تلاوته والوضوء لها وأن لا يقرأه الشخص وهو متنجس الفم فإنه مكروه وقيل: حرام كالمس باليد المتنجسة وكون القراءة في مكان نظيف والقارئ مستقبل القبلة متخشعا بسكينة ووقار مطرقا رأسه والاستياك لقراءته والترتيل والتدبر والبكاء أو التباكي وتحسين الصوت بالقراءة وأن لا يتخذه معيشة وأن يحافظ على أن لا ينسى آية أوتيها منه فقد أخرج أبو داود وغيره: عرضت عليّ ذنوب أمتي فلم أر ذنبا أعظم من سورة القرآن أو آية أوتيها رجل ثم نسيها وأن لا يجامع بحضرته فإن أراد ستره وأن لا يضع غيره من الكتب السماوية وغيرها فوقه وأن لا يقلب أوراقه بأصبع عليها بزاق ينفصل منه شيء فقد قيل بكفر من يفعل ذلك إلى أمور أخر مذكورة في محالها (روح المعاني 14/154)

[1] وندب لحافظ القرآن أن يختم في كل أربعين يوما في كل يوم حزب وثلثا حزب أو أقل كذا في التبيين في مسائل شتى من ختم القرآن في السنة مرة لا يكون هاجرا كذا في القنية (الفتاوى الهندية 5/317)

[2] شعب الإيمان للبيهقي، الرقم: 1859، قال العلامة العراقي رحمه الله في المغني عن حمل الأسفار صـ 323: إسناده ضعيف

[3] أفضل القراءة أن يتدبر في معناه (الفتاوى الهندية 5/317)

[4] سورة محمد: 24

About admin

Check Also

Sunna Na Adabu Za Dua 8

19. Jiepushe na ulaji wa haramu au chakula chenye mashaka na kujihusisha na madhambi. Mtu …