Umar (radhiya alaahu ‘anhu) Akiwaheshimu Azwaaj-ul-Mutahharaat (radhiyallahu ‘anhun)

Aslam (rahimahullah), mtumwa wa Umar (radhiyallahu ‘anhu), anaripoti kwamba Umar (radhiyallahu ‘anhu) alikuwa na sahani tisa maalum zilizohifadhiwa kwa ajili ya kutuma zawadi kwa Azwaaj-ul-Mutahharaat (wakezake na Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) na mama wa ummah.

Aslam (rahimahullah) alitaja kwamba wakati wowote chakula kizuri, tunda au nyama inapomjia Umar (radhiya allaahu ‘anhu), basi alikuwa akifanya hisa tisa, aziweke kwenye sahani tisa na kuzipeleka kwa Azwaaj-ul-Mutahharaat kwa heshima.

Alikuwa akipeleka sahani nane za kwanza kwa Azwaj-e-Mutahharaat na akituma sinia ya mwisho kwa binti yake mpendwa, Hafsah (radhiyallahu ‘anha).

Kuna wakati ikitokea kuwa na upungufu kidogo katika sinia yoyote, basi alikuwa akituma sahani hio kwa binti yake kipenzi, Hafsah (radhiyallahu ‘anha), na kuhakikisha kwamba wake wengine wa Mtume (sallallahu ‘alaihi wasallam) wanapokea sinia kamili. Kwa njia hii, Umar (radhiya allaahu ‘anhu) alitoa upendeleo kwa wake wa Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) kuliko familia yake mwenyewe. (Muwatta Imaam Muhammad #405)

About admin

Check Also

Uhuru wa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) na hamu ya Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam) kwa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) kuwa huru

Wakati mmoja, wakati akizungumza kuhusu Bilaal (Radhiyallahu 'Anhu), Sa'eed bin Musayyib (Rahimahullah) alisema:

Tamaa ya kuwa muisilamu ilikuwa kubwa sana moyoni mwa Bilal (Radi Allahu 'Anhu). Alikuwa akiwekwa chini na kuteswa katika mikono ya makafiri. Wakati wowote makafiri wangejaribu kumlazimisha kuachana na Uislamu, angekataa kwa nguvu na kutangaza waziwazi "Allah Allah" (yaani Allah Ta'ala ndiye mungu pekee anayestahili kuabudiwa).

Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) kisha alikutana na Abu Bakr (Radhiyallahu' Anhu) na alionyesha hamu yake akisema, "Ikiwa tu tungekuwa na mali ambayo tunaweza kumnunua Bilaal (na kumwachisha huru)!" Baada ya hapo, Abu Bakr (Radhiyallahu 'Anhu) alimkaribia 'Abbaas (Radhiyallahu' Anhu) akamwambia, "Nenda umnunue Bilaal kwa niaba yangu."