Abu Bakr (radhiyallahu ‘anhu) akijitolea Mali yake Kwa Sababu ya Rasulullah (Sallallahu ‘alaihi wasallam)

Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alisema: “Hakuna mali ya mtu iliyoninufaisha zaidi kama mali ya Abu Bakr (radhiyallahu’anhu).

Aliposikia hivyo, Abu Bakr (radhiyallahu ‘anhu) akaanza kulia na kusema, “Mali yangu yote na mimi pia ni wa kwako, Ewe Nabi Wa Allah (sallallahu ‘alaihi wasallam)!

Katika riwaya ya Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) ndani ya Musnad Ahmad, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) ametaja: “Hakuna mali (ya mtu yoyote) iliyoninufaisha kama mali ya Abu Bakr (radhiyallahu ‘anhu).

Kusikia hivyo, Abu Bakr (radhiyallahu ‘anhu) akaanza kulia, na kisha akasema mara tatu, “Ewe Rasulullah! Kwa hakika, ilikuwa kupitia kwako kwamba Allah Ta’ala amenibariki na kila kitu!”

About admin

Check Also

Ushujaa wa Abdullah bin Mas’uud (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Wakati wa vita vya Hunain, Waislamu walipata kushindwa kwa muda. Katika kipindi hiki kigumu, Abdullah …