Abu Bakr (radhiyallahu ‘anhu) akijitolea Mali yake Kwa Sababu ya Rasulullah (Sallallahu ‘alaihi wasallam)

Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) anaripoti kwamba Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) alisema: “Hakuna mali ya mtu iliyoninufaisha zaidi kama mali ya Abu Bakr (radhiyallahu’anhu).

Aliposikia hivyo, Abu Bakr (radhiyallahu ‘anhu) akaanza kulia na kusema, “Mali yangu yote na mimi pia ni wa kwako, Ewe Nabi Wa Allah (sallallahu ‘alaihi wasallam)!

Katika riwaya ya Abu Hurairah (radhiyallahu ‘anhu) ndani ya Musnad Ahmad, Rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam) ametaja: “Hakuna mali (ya mtu yoyote) iliyoninufaisha kama mali ya Abu Bakr (radhiyallahu ‘anhu).

Kusikia hivyo, Abu Bakr (radhiyallahu ‘anhu) akaanza kulia, na kisha akasema mara tatu, “Ewe Rasulullah! Kwa hakika, ilikuwa kupitia kwako kwamba Allah Ta’ala amenibariki na kila kitu!”

About admin

Check Also

Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) akiwa katika jukumu la kutunza mkuki wa Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam)

Mfalme wa Abyssinia (Najaashi (Rahimahullah) aliwahi kumtumia Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) mikuki mitatu kama zawadi. Baada ya kupokea mikuki mitatu, Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) aliimpa Ali (Radhiyallahu' Anhu) mkuki mmoja, akaampa Umar (Radhiyallahu' Anhu) mkuki wa pili na akabaki na mkuki wa tatu.

Katika vipindi vya laidi (idi ndogo na idi kubwa), Bilaal (Radhiyallahu 'Anhu) alikuwa akibeba mkuki wa Rasulullah (Sallallahu' Alaihi Wasallam) na kutembea mbele yake. Alikuwa akitembea mbele ya Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) wakati akiwa ameshikilia mkuki kwa kumheshimu Rasulullah (Sallallahu' Alaihi Wasallam).