Upendo wa Anas bin Nadhr (radhiyallahu ‘anhu) kwa Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) na kuwa kwake shahidi katika vita vya Uhud

Wakati Waislamu walipokuwa wanazidiwa katika vita vya Uhud, habari za uongo zilianza kuenea kwamba Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) ameuwawa. Hii habari zilisababisha wengi wa Maswahaba (radhiyallahu ‘anhum) kukata tamaa na kupoteza moyo.

Anas bin Nadhr (radhiyallahu ‘anhu) alitokea kumuona Umar (radhiyallahu ‘anhu) na Talhah (radhiyallahu ‘anhu) pamoja na kundi la Maswahaabah (radhiyallahu ‘anhum) katika hali ya huzuni na kukata tamaa kabisa. Akawaambia, “Kwa nini nawaoneni ninyi nyote hivyo kama wenye kukata tamaa na wenye huzuni?” Wakajibu, “ameuwawa.”

Anas (radhiyallahu ‘anhu) akasema, “Basi ni nani anapenda kuishi baada ya yeye kufa? Njooni, twende mbele na panga zetu na tuungane na mpenzi wetu, Nabii wa Allah (sallallahu alaihi wasallam)!” Muda aukupita Baada ya kutamka haya maneno yeye kujitumbukiza katika mistari ya maadui na kupigana kwa ujasiri mpaka akauawa kishahidi.

Anas (radhiyallahu ‘anhu) alikuwa na mapenzi ya hali ya juu sana kwa Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) mpaka hakuona maisha haya kuwa na thamani ya kuishi bila yeye. (Dalail un Nubuwah, 3/245)

About admin

Check Also

Uhuru wa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) na hamu ya Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam) kwa Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) kuwa huru

Wakati mmoja, wakati akizungumza kuhusu Bilaal (Radhiyallahu 'Anhu), Sa'eed bin Musayyib (Rahimahullah) alisema:

Tamaa ya kuwa muisilamu ilikuwa kubwa sana moyoni mwa Bilal (Radi Allahu 'Anhu). Alikuwa akiwekwa chini na kuteswa katika mikono ya makafiri. Wakati wowote makafiri wangejaribu kumlazimisha kuachana na Uislamu, angekataa kwa nguvu na kutangaza waziwazi "Allah Allah" (yaani Allah Ta'ala ndiye mungu pekee anayestahili kuabudiwa).

Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) kisha alikutana na Abu Bakr (Radhiyallahu' Anhu) na alionyesha hamu yake akisema, "Ikiwa tu tungekuwa na mali ambayo tunaweza kumnunua Bilaal (na kumwachisha huru)!" Baada ya hapo, Abu Bakr (Radhiyallahu 'Anhu) alimkaribia 'Abbaas (Radhiyallahu' Anhu) akamwambia, "Nenda umnunue Bilaal kwa niaba yangu."