Sahaabah

Ukarimu Mkubwa wa Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Mke wa Talhah (rahdiyallahu ‘anhu), Su’da bint ‘Awf al-Muriyyah alitaja tukio lifuatalo kuhusu mumewe Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu): “Siku moja, Talhah aliingia nyumbani katika hali ya dhiki. Nilipoona hali hii, nilimwambia, ‘Kwa nini ninakuona ukiwa na huzuni? Kuna nini? Je! nilifanya jambo ambalo limekuuzi hadi nakuona ukiwa umefadhaika? Tafadhali niambie …

Soma Zaidi »

Kupokea jina la Al-Fayyadh kutoka kwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam)

Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alimpa Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu) cheo cha Talhah Al-Fayyaadh (mtu mkarimu sana) mara kadhaa. Ifuatayo ni tukio moja kama hilo: Wakati wa vita vya Zi Qarad, Rasulullah (sallallahu alaihi wasallam) alipita karibu na kisima cha Baisaan. Maji ya kisima hiki yalijulikana kuwa machungu. Mtume (Sallallahu alaihi …

Soma Zaidi »

Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu) Akitimiza Ahadi Yake

Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu) anaripoti: Maswahaabah (Radhiya Allaahu ‘anhum) siku moja walimwambia bedui mmoja, “Nenda ukaulizie kutoka kwa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) kuhusu nani Allah Ta’ala Anayemkusudia (katika Aya ifuatayo ya Qur’an Majeed) “Miongoni mwao (Maswahaba) wapo waliotimiza ahadi zao (kwa Allah Ta’ala wa kubaki imara kwenye uwanja wa vita …

Soma Zaidi »

Talhah (Radhiyallahu ‘anhu) katika Vita vya Uhud

Jaabir bin Abdillah (Radhiya Allaahu ‘anhu) anasimulia: Siku ya Uhud, Maswahaba walipoanza kukimbia kutoka kwenye uwanja wa vita, Mtume (Sallallahu alaihi wasallam) aliachwa peke yake mahali fulani na maswahaabah kumi na mbili tu waliokuwepo pamoja naye. Miongoni mwa maswahaabah kumi na mbili alikuwepo Talhah ibn Ubaydillah (Radhiya Allaahu ‘anhu). Wakati …

Soma Zaidi »

Uislamu wa Talha bin Ubaidillah (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Siku ambayo Abu Bakr Siddeeq (Radhiya Allaahu ‘anhu) aliposilimu, alianza kuwalingania watu kwenye Uislamu. Allah Ta’ala alimfanya kuwa sababu ya Maswahaabah (Radhiya Allaahu ‘anhum) wengi kuingia katika Uislamu. Miongoni mwa maswahaabah waliosilimu kupitia kwa Abu Bakr Siddiq (Radhiya Allaahu ‘anhu) ni Talhah bin Ubaidillah (Radhiyallahu ‘anhu). Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu) …

Soma Zaidi »

Ukarimu Wa Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Ali bin Zayd (rahimahullah) anasimulia kwamba wakati fulani, Bedui mmoja alimwendea Talhah (Radhiyallahu ‘anhu) ili kuomba msaada kutoka kwake. Bedui huyo alikuwa ni ndugu wa Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu) na alipowasilisha ombi lake, alimuuliza kupitia uhusiano wa kindugu ambao wote wawili walishiriki baina yao. Talha (Radhiya Allaahu ‘anhu) akajibu, ‘Kabla …

Soma Zaidi »

Hofu Ya Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mali ya Dunia isimfanye Kuto kumcha Mwenyezi Mungu (subhaanahu wata’alah)

Wakati mmoja, Talhah (Radhiya Allaahu ‘anhu) alipokea dirham laki saba kutoka Hadhramawt. Usiku ule, alipopumzika ili alale, hakutulia, akigeuka huku na huko. Mke wake kuona wasiwasi wake, aliuliza, “Ni nini kinakusumbua?” Akajibu, “Mtu atawezaje kumfikiria Mola wake wakati ana mali nyingi nyumbani kwake? (yaani nahofia kuwa mali hii itasababisha nighafilike …

Soma Zaidi »

Talhah (radhiyallahu anhu) katika Vita vya Uhud

Zubair bin Awwaam (radhiyallahu anhu) anaripoti kwamba katika tukio la Uhud, Mtume (sallallahu alaihi wasallam) alivaa vazi la kivita mara mbili. Wakati wa vita, Mtume (sallallahu alaihi wasallam) alikusudia kupanda juu ya jabali lakini kutokana na uzito wa zile vazi mbili, hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo alimwomba Talhah (radhiyallahu anhu) …

Soma Zaidi »

Nafasi Ya Juu Ya Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu) Mbele Ya Abu Bakr (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Baada ya kufariki kwa Mtume (Sallallahu alaihi wasallam), Ma answaar walikuwa wamekusanyika huko Thaqifah Bani Saa’idah (bustani ya matunda ya Bani Saa’idah) kumchagua Khaleefah mpia kutoka miongoni mwao. Wakati huo, Abu Bakr na Umar (radhiyallahu anhuma) walikuwa nyumbani kwa Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) na walikuwa hawajui kinachoendelea. Wakiwa nyumbani, Umar …

Soma Zaidi »

Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) Akiuonyesha Ummah Nafasi Tukufu Ya Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) wakati fulani alikua amekaa pamoja na Abu Bakr (Radhiya Allaahu ‘anhu), Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu), Abu Ubaidah (Radhiyallahu ‘anhu) na Maswahaba wengineo (Radhiyallahu ‘anhum) na kinywaji kikaletwa kwa Nabi (Sallallahu alaihi wasallam). Nabi (Sallallahu alaihi wasallam) alichukua kinywaji hicho mkononi mwake na akampa Abu Ubaidah (Radhiyallahu …

Soma Zaidi »