Sa’d bin Abi Waqqaas (radhiyallahu ‘anhu) akishiriki katika Ghusal ya Sa’eed bin Zaid (Radhiyallahu’ Anhu)

Wakati Sa’eed bin Zaid (Radhiyallahu ‘Anhu) alipofariki, sa’d bin abi Waqqaas (Radhiyallahu’ Anhu) na Abdullah bin Umar (Radhiyallahu ‘Anhuma) walikuwa miongoni ya watu waliompa Ghusal.

Baada ya Janazah kubebwa na watu kutoka Aqeeq kwenda Madinah Munawwarah kuzikwa huko Baqi ‘, kaburi la Madinah Munawwarah. Pindi Janaazah ilipopita nyumba ya Sa’d (Radhiyallahu anhu), Sa’d (Radhiyallahu anhu) alingia nyumbani kwake kuoga kabla ya kujiunga na watu katika janazah.

Kabla ya kuondoka nyumbani kwake, aliwambia familia yake kw kusema, “Sikuoga kwa sababu nilishiriki katika Ghusal ya Sa’eed (Radhiyallahu ‘Anhu). Badala yake, nilioga tu kwa sababu ya joto.” (Majmauz Zawaaid, #14880)

About admin

Check Also

Muaaz (Radhiya Allaahu ‘anhu) Akivunja Sanamu la Amr bin Jamooh (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Katika mwaka wa 13 baada ya nubuwwah, watu 70 kutoka Answaar walikuja kuhijji na kusilimu …