Nafasi ya hali ya juu ya Sa’eed bin Zaid (Radhiyallahu ‘Anhu) Mbele ya Abdullah bin Umar (Radhiyallahu ‘Anhuma)

Katika tukio moja, wakati Abdullah bin Umar (Radhiyallahu ‘Anhuma) alikuwa akijiandaa kwenda katika kuswali Jumuah, alisikia Kwamba mjomba wake, Sa’eed bin Zaid (Radhiyallahu ‘Anhu) alikuwa mgonjwa sana na alikuwa kwenye sakaratul mauti.

Habari hii ilimfikia wakati alikuwa tayari amepaka manukato kwenye mwili wake na alikuwa karibu kuondoka nyumbani kwake kwenda kuswali Jumuah.

Lakini, aliposikia habari hii, mara moja akapanda mnyama wake na badala ya kwenda kuswali Jumuah, akaelekea Aqeeq, mahali ambapo Saeed (Radhiyallahu ‘Anhu) aliishi. Aqeeq ilikuwa mahali mbali na mji, ambapo swalaah ya Jumuah haikuwa ya lazima kwa watu wanaoishi huko, kwa sababu sharti ya wajibu wa Jumuah hazikupatikana.

Abdullah bin Umar (Radhiyallahu ‘Anhuma) alikwenda Aqeeq na kusaidia katika kumpa Ghusal Sa’eed (Radhiyallahu’ Anhu). Baada ya kumpa Ghusl, alimfunika ndani ya sanda na akajiunga na watu katika kutekeleza swalaah ya Janaazah.

About admin

Check Also

Bilaal (Radhiyallahu ‘Anhu) akiwa katika jukumu la kutunza mkuki wa Rasulullah (Sallallahu’ Alaihi Wasallam)

Mfalme wa Abyssinia (Najaashi (Rahimahullah) aliwahi kumtumia Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) mikuki mitatu kama zawadi. Baada ya kupokea mikuki mitatu, Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) aliimpa Ali (Radhiyallahu' Anhu) mkuki mmoja, akaampa Umar (Radhiyallahu' Anhu) mkuki wa pili na akabaki na mkuki wa tatu.

Katika vipindi vya laidi (idi ndogo na idi kubwa), Bilaal (Radhiyallahu 'Anhu) alikuwa akibeba mkuki wa Rasulullah (Sallallahu' Alaihi Wasallam) na kutembea mbele yake. Alikuwa akitembea mbele ya Rasulullah (Sallallahu 'Alaihi Wasallam) wakati akiwa ameshikilia mkuki kwa kumheshimu Rasulullah (Sallallahu' Alaihi Wasallam).