Ushujaa wa Zubair (Radhiya Allaahu ‘anhu)

Siku ya (vita) vya Yarmuk, Maswahabah (Radhiya Allaahu ‘anhum) walimwambia Zubair (Radhiya Allaahu ‘anhu): “Kwa nini huwashambulia maadui kwa ijtihada zote, nasi tutakufuata katika kuwashambulia ?”

Zubair (Radhiya Allaahu ‘anhu) akajibu, “Najua kwamba nikiwashambulia na ijtihada zote, nyinyi hamtaungana nami.

Maswahaabah (Radhiya Allaahu ‘anhum) wakasema, “Hapana, tutaungana nawe.”

Zubair (Radhiya Allaahu ‘anhu) hivyo alipenya kwenye mistari ya maadui akipigana nao. Aliendelea kupigana na maadui mpaka akafika mwisho wa upande wa maadui na hakuna hata mwenzake mmoja aliungana naye hadi wakati huu.

Basi alipoanza kurejea (kurudi upande wa Waislamu), maadui wakashika hatamu ya farasi wake na wakampiga mara mbili (na panga zao) begani. Mbali na majeraha haya mawili (aliyoyapata katika vita vya Yarmook), kulikuwa na jeraha lingine kati ya majeraha haya mawili yaliyosababishwa na kupigwa kwa upanga, ambayo aliipata siku ya Badr alipokuwa akipigana.

Baada ya kutaja hayo hapo juu, Urwah (rahimahullah) alisema, “Nilipokuwa mtoto, nilipokuwa nikicheza, nilikuwa nikiweka vidole vyangu kwenye matundu (ya ngozi ya bega lake).

Siku hiyo (ya Yarmouk, kaka yangu) Abdullah bin Zubair (radhiyallahu ‘anhu) pia alikuwa pamoja naye (baba yetu, Zubair (Radhiya Allaahu ‘anhu) naye alikuwa na umri wa miaka kumi wakati huo. Zubair (Radhiya Allaahu ‘anhu) akamuweka juu ya farasi na akamchagua mtu wa kumtunza (akiwa hayupo wakati wa vita). (Swahiyh Bukaari #3975)

About admin

Check Also

Abu Ubaidah (Radhiya Allaahu ‘anhu) Apoteza Meno Yake Katika Vita Vya Uhud

Wakati wa vita vya Uhud, Rasulullah (Sallallahu alaihi wasallam) alishambuliwa na maadui na viungo viwili …