Umuhimu Wa Kujiunga Ili Upate Usahihi Wa Aqiidah

Dini ya Uislamu pamoja na nguzo zake zote, hutegemea msingi wa imani na imani sahihi. ikiwa imani ya mtu sio sahihi, lakini haitamfanya atoke kwenye zizi la Uislamu, basi hata kama anaweza kujitahidi kutekeleza matendo ya uadilifu na ya haki, hatapokea ahadi zilizoahidiwa kama imani yake ambayo ni msingi wa matendo yake, sio sahihi.

Ikiwa imani ya mtu inapingana na imani ya kimsingi ya Uislamu (imani za kimsingi ambazo zinahitajika kwa mtu kuwa Mwislamu), basi hatakama kwa nje anaonekana kuwa muumini na anafanya mila ya Uislamu pamoja na Waislamu, kwa sababu hatekelezi msingi za Uislamu hatopata thawabu yoyote kwa matendo yake mema kwa sababu ikiwa yeye sii muumini.

Kuhusu mtu ambaye hana imani, Allah anaeleza katika Quran:

مَثَلُ الَّذِينَ كَفَرُوا بِرَبِّهِمْ اَعْمَالُهُمْ كَرَمَادِ نِ اشْتَدَّتْ بِهِ الرِّيحُ فِي يَوْمٍ عَاصِفٍ ؕ لَّا يَقْدِرُونَ مِمَّا كَسَبُوا عَلىٰ شَيْءٍ ؕ ذٰلِكَ هُوَالضَّلٰلُ الْبَعِيدُ ﴿سورة ابرٰهيم: ١٨﴾

Mfano ya wale ambao wanaomkana mola wao ni kama majivu yanayopeperushwa na upepo siku ya dhoruba. hawatopata chochote (malipo yoyote ya matendo mema) ya waliyo yachuma. hiyo ndio hatua ya mbali zaidi ya kupotea mbali na njia sahihi.

Katika aya nyingine ya quraan, Allah subhaana wata’ala anasema:

قُلْ هَلْ نُنَبِّئُكُم بِالْاَخْسَرِينَ أَعْمَالًا ﴿١٠٣﴾ الَّذِينَ ضَلَّ سَعْيُهُمْ فِي الْحَيٰوةِ الدُّنْيَا وَهُمْ يَحْسَبُونَ اَنَّهُمْ يُحْسِنُونَ صُنْعًا ﴿١٠٤﴾ أُولٓـٰئِكَ الَّذِينَ كَفَرُوا بِاٰيٰتِ رَبِّهِمْ وَلِقَآئِهِ فَحَبِطَتْ اَعْمَالُهُمْ فَلَا نُقِيمُ لَهُمْ يَوْمَ الْقِيٰمَةِ وَزْنًا ﴿١٠٥﴾ ذٰلِكَ جَزَآؤُهُمْ جَهَنَّمُ بِمَا كَفَرُوا وَاتَّخَذُوا اٰيٰتِي وَرُسُلِي هُزُوًا ﴿سورة الكهف: ١٠٦﴾

Sema: Je! tukujulishe wale walio khasiri zaidi kwa matendo yao (hao ni) wale ambao juhudi zao zimepotea katika maisha haya huku wakidhani kwamba wanapata mema kwa matendo yao. Hao ndio waliokuwa wakikanusha aayaa (uthibitisho, Aya za quraani na Ishara za Allah subhaana wata’ala) za Mola wao na kukutana naye (huko Akhera). Ndivyo matendo yao ni bure, na siku ya kuamrishwa, hatutazipatia uzito wowote (kwa matendo mema waliyoyafanya ulimwenguni). Hiyo ndiyo malipo yao ya jahannam – kwa sababu walikanusha na wakazichukua Ishara zangu na Mitume wangu kuwa ni mzaha na dhihaka.

Kutoka kwa aya hapo juu, tunahitimisha kuwa bila Imaan, mtu hatokuwa muumini.

Imaan ni kuamini kanuni za kimsingi za imani kama umoja wa Allah subhaana wata’ala kuamini sifa zake zote, mwisho wa utume wa rasulullah (sallallahu ‘alaihi wasallam), utume wa ambiyaa (‘alaihimus salaam) wote, uwepo kwa malaika, maandishi ya wahi, imani yataqdeer (kuamuliwa kabla), kutokea kwa siku ya qiyaama na maisha baada ya kifo, uwepo wa jannah na jahaannum n.k.

Ikiwa mtu anaswali tuu, anatoa zakaah, anafunga katika mwezi wa Ramadhaan, anahiji nk, lakini haleti imaan katika misingi ya imani, hatachukuliwa kama Mwislamu. kwa hivyo, ni muhimu kwa mtu kusoma Uislamu kwa usahihi na kujifunza misingi ya imani za Uislamu ili mtu aweze kuwa muumini wa kweli na kupata thawabu zilizoahidiwa kwa matendo mema, na pia kupata ukaribu wa allah.

About admin

Check Also

Imani kuhusu Malaika

1. Malaika ni viumbe vya Allah subhaana wata’ala visivyo na dhambi na wameumbwa kutokana na …